Beki wa timu ya taifa ya Ufaransa Raphael Varane na klabu ya Mnchester United amerejea kwenye kikosi cha kwanz cha kocha Didier Deschamps dhidi ya timu ya taifa ya Denmark leo katika mchezo wa pili wa kundi D.
Beki huyo ambaye hajaonekana uwanjani toka mwezi oktoba ambapo alipata majeraha akiwa anaitumikia klabu yake ya Man United dhidi ya klabu ya Chelsea katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza ataonekana leo uwanjani kwa mara ya kwanza.
Varane alikosekana katika mchezo wa kwanza mabao timu hiyo ilicheza dhidi ya timu ya taifa ya Australia na kupata ushindi wa mabao manne kwa moja, Na leo hii atashuka dimbani huku Ufaransa ikiwa inatafuta nafasi ya kufuzu hatua ya 16 bora dhidi ya Denmark.
Raphael Varane amekua mwanajeshi mtiifu wa kocha Deschamps kwa muda mrefu kwani kwenye kwenye mabeki wa katikati walioitwa kwenye kikosi hicho ni Varane pekee aliebakia wakati timu hiyo inatwaa kombe la dunia 2018 pale Urusi.
Timu ya taifa ya Ufaransa itakumbana na mtihani mzito kwani Denmark ni miongoni mwa timu ambazo zimekua zikisumbua timu hiyo kwani hata kwenye michuano ya ulaya maarufu kama Uefa Nations League ambapo walikua kundi moja Ufaransa kuambulia kipigo michezo ypote miwili.

Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.

