Baada ya kudumu kwenye kikosi cha Manchester United kwa miaka 8. Ashley Young aliamua kujiunga na Inter Millan mapema mwezi Januari.
Young ambaye alikuwa na wakati mzuri ndani ya kikosi cha Manchester United. Alijikuta akiwa katika wakati mgumu baada ya Ole Gunnar Solskjaer kukabidhiwa mikoba ya Mourinho.

Ujio wa Solskjaer ulileta neema kwa wachezaji vijana huku wachezaji wenye umri mkubwa wakitumika mara chache sana. Young (35) alijikuta kwenye wakati mgumu zaidi baada ya ujio wa Aaron Wan Bissaka na kuchipukia kwa Brandon William, nafasi za vijana hawa zilimfanya Young kukosa namba kwenye kikosi cha Manchester United.
Akizungumzia suala hilo wakati alipofanya mahojiano na ukurasa wa Uefa, Young amenukuliwa akisema, ” Kuwepo kwangu England maisha yangu yote, kiukweli yalikua ni mabadiliko makubwa. Ilikuwa ni fursa yangu ya kwenda kucheza mara kwa mara.”

” Nilizungumza na Ole na alinambia sitokuwa nikicheza mara kwa mara kama nilivyokuwa ninahitaji. Ukiwa unaelekea mwishoni mwa muda wako wa kucheza soka, unahitaji kuwa unacheza mara kwa mara. Nipo vizuri kama wachezaji wengine na bado ninavitu vingi vya kuonesha.
“Kwa upande wangu umri ni namba tu. Ole alisema atawapa nafasi wachezaji vijana na hivyo sitokuwa na nafasi kubwa. Fursa ya kujiunga na Inter ilipokuja, ilikuwa ni jambo rahisi kwangu. Nilihitaji kupanda ndege na kuondoka eneo lile [Man United] mapema kabisa.

“Nilikuwa nikizungumza na kocha pamoja na wachezaji wa hapa [Inter Millan] niliokuwa ninawafahamu. Ilikuwa ni fursa nzuri, moja ya klabu kubwa duniani katika ulimwengu wa soka.”
Katika kuelekea mchezo wao wa nusu fainali dhidi ya Shaktar Donetsk, Young amezungumzia namna ya ufundishaji wa kocha wake – Antonio Conte.
“Conte anahitaji kila kitu, sio uwanjani tu hata kwenye mazoezi. Unaweza kusema ni mshindi, anahitaji ushindi na anataka hilo litimizwe na kila mchezaji. Kila mmoja ana akili ya ushindi.

” Serie A ni ligi inayotumia sana mbinu kuliko nilivyokuwa nimezoea, lakini ni moja ya vitu unapaswa kuvizoea na ninadhani nimeshazoea. Kucheza kama winga mkabaji kunahitaji mbio nyingi na kushambulia, ni vitu ambavyo nimevizoea na imenisaidia kufunga magoli na kutoa pasi za magoli.
“Nilipokuwa Man United, nilikuwa kama mlinzi zaidi. Ukiwa hapa [Inter] unapaswa kuwa unashambulia zaidi kuliko kukaba.”

Akiwa Manchester United, Young alibeba makombe 5 likiwemo ya Ligi Kuu Uingereza- EPL. Pia, alikabidhiwa unahodha wa timu hiyo baada ya Antonio Valencia kuondoka Old Trafford. Inter Millan walimsajili kwa ada ya euro milioni 1.5 kabla hakuwa mchezaji huru.
Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Basi fahamu kuwa kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.


Omary lukumbi
Young hakua mbaya ila umri aliokua nao na mara nyingi alikua anatoa boko sana
Ester jackson
Habari njema sana
Angelina
Goodnews
Venerose
Habari njema kwetu
Rose kapinga
Meridianbet mpo vizur!!!!
rama
Maoni:hata ivyo inter sio timu ndogo
Theonestina
Sawa
Mwajumah
Habari njema sana#Meridianbettz
Dorophina
Habari njema hizi
Adelta
Young Yuko vizuri
@meridianbettz
Zeiyana
Ashley young alisumbua sana kipindi kile alivyo kua man Chester utd..!kwa mri alio kua nao sasa hivi me sioni kama hamefikia mri mkubwa hadi kufikia yeye kuona so wanapo ingia wachezaji chipukizi kikubwa angalie tu kuna mchezaji amabaye hanayeweza kufikia kiwango chake
Fatina mfingi
Bado yupo vizur!!
aisha
Young ni mchezaji mzuri sana basi tuu muda wake ukifika asijali nyota yake itang,ara
Samiah
Sawa
Mwanahamisi
Mpo juu meridianbet
Sabrina
Bado young anadai kabisa hakipangwa kikosoni bora alivyoenda inter
Caroline
Young Hana shida mbona
Sauda
Mpo vizuri kwa taarifa
Lydia Emmanuel Magoti
Yaung yupo vizuri
Tatu
Hapo ndio panakufaa kijana
felister
even if inter sio timu mbaya
Ernest
Shughuli ya Young wanaijuwa huko Italia, Amekuwa msaada mkubwa sana kwa Inter
Njiku
Safii sana young we kipute inter waache man u wakigwaya gwaya na timu lao bovu lisilo LA ushindani
Sadick
Kweli umri ni namba tu kama alivyosema mwenyewe Ashley Young kwa maana siku za karibuni amekuwa moto wa kuotea mbali pamoja na umri wake kuwa mkubwa. Niliona akifunga magoli mawil kwenye mechi ya Inter dhidi ya mshindi wa tatu ktk Ligi Atalanta#meridianbettz
Nasra
Italy ndo inchi ambayo inawatumia Sana wakongwe kwenye soka la miguu.
Saupha mohamed
Kijana anajua
Shafii
Kwa tunavyo faham ligi ya inter awaangaliagi umri isipo kua uwezo ukiruhusu unacheza.
Issa
Young amekuw kwenye kiwango bora toka atue inter
Janeflora malisa
Inter wanaangalia uwezo wa mtu
Furahav
Habari nae.
Devotha
Young ni mchezaji mzuri
Hope mwaikuka
Namkubali sana
Povel
Habar njema
David Pere
Safii sana young we kipute inter waache man u wakigwaya gwaya na timu lao bovu lisilo
farida ahmadi
Safii Sana Ashley Young
warda
Kapotea huyu kwenye Gemu#Meridianbettz
magdalena
young yupo sahihi juu ya alisemalo bado yupo vizuri katika soka
Gabriel
Young yuko vzur sana namkubal
Shan
Serie A hua wanaangalia uwezo wa mchezaji sio umri.