Hansi Fick atamrithi Joachim Low kama kocha wa Ujerumani baada ya Mashindano ya Ulaya ya msimu wa joto kumalizika.
Baada ya kumalizana na Bayern Munich mwishoni mwa msimu wa Bundesliga, Flick alikuwa anatarajiwa kuchukua nafasi na timu ya taifa ya Ujerumani.
Uteuzi wake ulithibitishwa Jumanne asubuhi, na atajiunga na kandarasi ya miaka mitatu ambayo itaendelea hadi 2024, baada ya Mashindano ya Ulaya yaliyoandaliwa nchini Ujerumani.
Flick atapata euro milioni 6.5 kila mwaka na Ujerumani, chini ya ile aliyokuwa akilipwa Bayern.
Rais wa Barcelona Joan Laporta alikuwa akivutiwa na Flick hadi kuteuliwa kwake na Ujerumani kuwa rasmi. Flick, hata hivyo, alikuwa tayari amefikia makubaliano na Chama cha Soka cha Ujerumani.
BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.
Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.