Hadithi nzima inaanzia ile jioni ya Agosti 3 mwaka 1999, waingereza walisimama kwa butwaa kubwa sana mitaa ya Longford London kumshangaa kijana mmoja mdogo sana aliyekuwa akiongozana na Arsene Wenger kuelekea maeneo ya Holloway yalipo makao makuu ya club ya Arsenal.

Mashabiki wengi wa Arsenal walihuzunishwa na usajili ule wakiamini Thierry Henry hakuwa na hadhi ya kucheza Arsenal, ila Wenger aliamua tu kumbeba kwa sababu alikuwa mfaransa mwenzake. Mitaa haikuwa inampa uzito sana. Wengi Jioni ile, walikuwa bize na ujio wa Davor Suker kutoka Real Madrid.

Walitazamana tu wakiambiana, “Si amefeli Juventus huyu mtoto? Jamani, kwani Arsenal ina shida winga? Hawa wafaransa wanabebana sana hawa.” Ila Wenger alimnong’oneza kwa kifaransa kijana wake ‘c’est la vie’ akimaanisha ‘ndiyo maisha jikaze.’
Ila laiti kama waingereza wangejua kuwa mzee Wenger kaleta ‘moto kama wa Sodoma’ kwa mabeki na makipa, wasingesema hovyo ile siku. Wenger alimuhamisha Henry kutoka eneo ka winga na kumfanya mshambuliaji wa kati. Kila mtu anajua nini kilifuata baada ya hapo.

Miaka nane aliyocheza Arsenal amepiga mabao 228, 175 yakiwa ya ligi. Mpaka kesho anabaki kuwa mfungaji wao bora wa muda wote. Amechukua mataji manne pale. Ameondoka na kiatu cha mfungaji bora wa msimu mara nne na amekuwa mchezaji bora wa mwaka mara tatu. Aliikosakosa ballon d’or ya 2003. Henry mtu bwana🙌.

Maisha yalienda kasi na Arsenal ilivurugika, ikapoteza ule uimara wake. Henry alivumilia kwa kuwa alipendana sana na Arsenal. Zaidi ya yote alimuheshimu sana Wenger. Ila Siku moja ya mwaka 2007 uzalendo ulimshinda. Henry akamfuata Wenger mazoezini na kumuambia. “Tuna timu nzuri sana ya vijana, ila najua hatuwezi kuchukua taji la ligi kwa sasa. Nina miaka 31, siwezi kusubiri vijana wakomae. Naomba niondoke, nikajaribu kushinda sehemu nyingine.”

Hivo ndivyo Henry alivofika Barcelona. Alienda kutwaa la liga mbili na UEFA mwaka 2009. Mpaka leo Henry anadai kuondoka Arsenal ndiyo maamuzi magumu kuwahi kuyafanya katika maisha yake. Si rahisi kuagana na watu mliowekana moyoni kwa ajili ya mafanikio binafsi.
Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.


Ernest
Aubameyang kasikai Call wahuni wanasema , Ngoja tuone nini ataamua kwenye career yake
Njiku
Kweli kabisa henry alikuwa anauzalendo na timu yake na kumuheshimu sana kocha wake Wenger ila naona kama anampa Congo Pierre kwa kutaka kusepa klabuni hapo
Lydia Emmanuel Magoti
Mamuzi yake yalikuwa mazuri Henry kwalicho kiamua kutimukia Barcelona alikuwa mpamba naji Sana namuherewa sana
Tatu
Henry akikuwa MTU mwenye uzalendo na timu yake
warda
Henry Alikipiga sana Enzi zake#Meridianbettz
Mwajumah
Maamuzi yake yalikua mazuri Henry kwa alicho kiamua kutumikia barcelona#Meridianbettz
felister
kweli kabisa Henry huo ulikua ni uamuzi mgumu na ni wachache sana wenye moyo kama wako
Dorophina
Henry alikuwa mtu mwenye uwezo kipindi hicho na kipaji
Zeiyana
Daaah..!ulikua wakati mgumu sana kwa Wenger kipindi kile. Sizani kama arsenal watamuachia aubameyang asepe klabuni pale
Latifa juma mohamed
Henry akikuwa MTU mwenye uzalendo na timu yake
Shafii
Mi nadhani hata auba kwa umri aliokua nao anafikilia kwenda sahemu nyingine kutimiza ndoto zake.
Sadick
Aubameyang bado hajafikia uwezo wa kujitolea aliokuwa nao Henry#meridianbettz
Samira
Wamuacha auba aende sehemu nyingine akatimize ndoto zake
aisha
Henry alikua mtu mbaya sana Enzi zake
Fatina mfingi
Makal nzur
Neema
Mambo ya zamanii yanakupa historia. Henry alikuwa fitii mno
Janeflora malisa
Yupo fiti sana
Nasra
Sioni ata uwezo wake
Rehema
Bonge la makala
Theckla
Henry alikuwa na moyo wa peke ake
Caroline
Kazi ipo
Issa
Auba ndio mshambuliaji alieipaisha arsenal msimu huu
Povel
Duh makala noma sana hiiii
Khadija
Herny alikuwa mwenye uwezo kipindi hicho
Mwanahamisi
Kazi ipo
Adelta
Mashabiki tunashukuru kwa makala
@meridianbettz
Saupha mohamed
Henry alikua vizuri sana
Furahav
Hii makala inatufundisha kwamba husimzarau mtu usiyemjua.
Hope mwaikuka
My fav player of all time
Revina
Hiyo ndo waswahili wanasema usimzarau mtu usiemjua ,au hutakiwi kujitangaza vitendo vyako ndo vitawahabarisha hata asiekujua jina lakini kitendo chako tu atajua ,si yule aliefanya kitu flani ?
Gabriel
Sasa hapa Henry anamfundisha vibaya aubameyang nae afanye maamuz ya kuondoka Arsenal me namshauri asipokee simu
Sabrina
Duuh hatari
Devotha
Aubameyang kwa sasa hawezi kuondoka arsenal
Asia Abdy
Hee sio poa
Salma ngende
Jeshi LA zamani
Omary lukumbi
Safi sana tumeona hata kwa roben van persie vile vile kaja united kanyayua ndoo
Ester jackson
Habari nzuri sana
Samiah
Habari njemaaa
farida ahmadi
Yuko sahihi kabisah Henry
David Pere
Mi nadhani hata auba kwa umri aliokua nao anafikilia kwenda sahemu nyingine kutimiza ndoto zake.
magdalena
henry alikuwa na moyo wa kipekee sana ukiacha mbali na kipaji chake atakumbukwa sana pale barcelona
Shan
Kila mchezaji hua ana ndoto kwenye career yake ya mpira.
Tumaini kasalile
Safi