Herrera: Mbappe na Neymar Wanafuraha PSG

Ander Herrera amesisitiza kuwa Mbappe na Neymar wanafuraha sana pale PSG na klabu haina mpango wa kuwauza, zaidi ya kuwanunua mastaa wengine.

Mbappe na Neymar, kwa pamoja wamekuwa wakihusishwa na kuondoka klabuni hapo, huku klabu za Real Madrid na Barcelona zikihusishwa zaidi kuwania saini zao.

Lakini kwa mujibu wa Herrera, fowadi hawa wanaonekana kuwa na furaha zaidi pale PSG baada ya kuwasaidia timu yao kuchukua ubingwa wa Ligue 1 kwa mara ya 3 mfululizo.

Herrera akizungumza na AS, aliulizwa pia ikiwa klabu ikalazimika kumuuza mmoja wao, ni yupi kati ya wawili hawa itakuwa siyo rahisi kumbakiza?

Herrera: Mbappe na Neymar Wanafuraha PSG
Kylian Mbappe na Neymar

“Sifahamu, kwa kuwa sielewi wanalipwa kiasi gani au ni mapato ya kiasi gani wanayoiingizia klabu, ambayo pia ni kampuni.”

“Lakini nafahamu kuwa wao ni sehemu muhimu zaidi katika mradi na ninawaona wanafurahia kuwa na PSG.” -Ander Herrera

Ikumbukwe PSG walimshusha Neymar klabuni hapo kwa ada iliyovunja rekodi ya dunia ya €222M akitokea Barcelona mwaka 2017. Na sasa Barcelona wanataka kumrejesha kondoo waliyemuuza kwa mkulima mwingine wakiona bado amenona.

Wakati huo Mbappe alijiunga na klabu hiyo mwaka uliofuata baada ya Neymar kwa mkataba wa kudumu akitokea Monaco kwa ada ya €135M.

Wamekuwa sehemu muhimu ya PSG, na PSG wana jeuri ya pesa kuendelea kuwabakiza klabuni hapo licha ya kuripotiwa kwa nyakati tofauti kuwa mastaa hao wanatamani kuondoka.

Unafikiri PSG wamuuze nani na kumuacha yupi? Nitafurahi kusoma maoni yako hapo chini.

 


Bashiri Mechi za Leo Bundesliga BETI HAPA

54 Komentara

    Km wanafuraha wote wawili kuwepo PSG wawaache tu mpk watakapoamua wenyewe kuondoka

    Jibu

    Nafkili waache wote hapo PSG had watakapoana muda wao umeisha

    Jibu

    Safi Sana Kama wanafurahi waendee kubaki hukohuko

    Jibu

    Ni vizuri sana wakiwa na furaha

    Jibu

    Muunganiko wao ni mzuri itakuwa Poaw

    Jibu

    Wabak hapo hapo tu

    Jibu

    Mwamba wawili wamekutana sasa PSG mambo mubashara wapizani mjipange sasa

    Jibu

    Kuwa na furaha ni jambo la msingi ila waonyeshe uwezo wao kutokana na viwango kushuka has a kwa Neymar

    Jibu

    Kama wanafuraha waendelee kukaa hukohuko

    Jibu

    kama kumuuza wamuuze mbappe wamuache neymar ila mm Kama mm ningependa wote wabakie apo apo PSG

    Jibu

    Wabaki tu

    Jibu

    Kama wana furaha wabaki hapo hapo

    Jibu

    Hamna wakumuuza nafurahi kuona wanamfanya kazi pamoja

    Jibu

    Ni kweli wanafuraha na walipo kwa sasa na ndo maana wana fanya vizuri mtu anatakiwa kufurahia alicho nacho na alipo kwa wakati huo ili mambo yawe sawa

    Jibu

    ni kweli kabisa neymar na mbappe ni sehemu muhimu sana pale PSG na ndomana hawataki kuwaachia

    Jibu

    PSG wana jeuri ya pesa kuendelea kuwabakiza klabuni hapo

    Jibu

    Wasiende popote wabaki wawe pamoja

    Jibu

    Wameipa heshima zaidi PSG hawajutii kuwa pale ndo maana wanafurahia kuwepo

    Jibu

    Wote wauzwe tu mie sina hata faida#Meridianbettz

    Jibu

    Safi Sana waendelee kukaa
    PSG

    Jibu

    Hao ni kama mapacha 3..hawana sababu ya kwenda popote..hapo psg ndo furaha yao

    Jibu

    Safi Sana waendelee kukaa PSG

    Jibu

    Wauzwe tuu sina faida nao#meridianbettz

    Jibu

    Safi sana waendelee kukaa psg

    Jibu

    Kwa mtazamo wake yeye anawaona wana furaha lakini nikweli neymar hana fraha pale PSG

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Mbape angeenda Madrid ingekua poa sana

    Jibu

    Ander Herrera angekumbuka msemo wa Waswahili unaosema usiusemee moyo. Naamini Mbappe na Neymar wakipata timu kubwa inayoweza kuwanunua wanahama#meridianbettz

    Jibu

    herrera asiwasemee watu bhn

    Jibu

    Me sitaki auzwe mchezaji yeyote kati yao kwasababu wote wako kwenye nafasi nzuri na wala hawana mpinzani.

    Jibu

    Waendelee tu kubakia hapo ambapo ushindan ni wa kawaida majukumu yao sio makubwa sana ukilinganisha na timu kama Manchester united etc

    Jibu

    Mafundi wa mpira#meridianbettz

    Jibu

    Ni vizuri Sana Kama wanakuwa na furaha

    Jibu

    Mbape kweli fraha anayo lakini si kwa Neymar Hana furaha pale Ndio maana anataka kuondoka

    Jibu

    Gud Kama wataendeleah kusalia kwny viunga hvy vya prince stadium

    Jibu

    Haya ndo majembe yanayoisimamisha Chelsea

    Jibu

    Haya ndo majembe yanayoisimamisha PSG

    Jibu

    Hiyo ni jeuri ya pesa,ndiomaana wako na furaha

    Jibu

    Wabaki tuu

    Jibu

    Wamekuwa sehemu muhimu ya PSG lazima wafurahie na kujivunia viwango vyao#meridianbettz

    Jibu

    gud newz asante

    Jibu

    Ni vema ukabaki tu hapo hapo

    Jibu

    Wanapenda timu yao

    Jibu

    PSG kumenoga wababe wawili kukutana katika timu moja

    Jibu

    Sizani kama PSG itakua tayali kuwauza mastaa hao

    Jibu

    Wapo vizuri wanajua Nini wanakifanya ndomana wanajikuba Sana Fundi mpila awaoneani kinyongo awanyimiani pasi

    Jibu

    Safi Sana soccer lenye mafanikio linaleta matumaini uwanjani

    Jibu

    Wote wako vizur.nawakubar

    Jibu

    Habari mjema

    Jibu

    Nihabari njema sana hz

    Jibu

    Mafundi wa mpira wabaki waendelee kuiinua PSG

    Jibu

    Makala bomba na meridianbet

    Jibu

    Tunategemea makubwa kutoka kwao

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.