Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Isco Alacorn leo atarejea katika uwanja wa Santiago Bernabeu yalipo maskani ya Real Madrid ambapo utapigwa mchezo kati ya Real Madrid wakiwa nyumbani kuwakaribisha Sevilla.
Mchezaji huyo wa zamani wa klabu hiyo atarudi Bernabeu kama mchezaji wa Sevilla ambapom alijiunga na klabu hiyo majira ya joto dirisha lililopita huku kiungo huyo anarudi klabuni hapo kama gwiji kutokana na mafanikio aliyoyapata.
Kiungo Isco ambaye anaitumikia klabu ya Sevilla kwasasa ni mchezaji mwenye heshima ndani ya Real Madrid akihudumu kwa takribani miaka tisa baada ya kujiunga klabuni hapo Juni 2013 na kuondoka Julai 2022.
Isco ni miongoni mwa wachezaji tisa waliofanikiwa kubeba mataji matano ndani ya Real Madrid na historoa ya klabu hiyo itamkumbuka kama miongoni mwa wachezaji wenye mafanikio zaidi klabuni hapo.
Real madrid watakua uwanjani kumenyana na Sevilla leo na wakihitaji ushindi ili kuendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi kuu nchini Hispania.

