Serengeti Girls Wang’olewa Kishujaa Kombe la Dunia

TIMU ya Taifa ya Wasichana wa U17, Serengeti Girls imeyaaga mashindano ya kombe la dunia kishujaa baada ya kuchapwa mabao 3-0 mbele ya Colombia ambao kwa ushindi huo wamekwenda nusu fainali.
Serengeti Girls
Serengeti Girls

Kikosi hicho cha Bakari Shime kilimaliza mechi hiyo ya robo fainali wakiwa nane uwanjani kufuatia wachezaji wawili kupewa kadi nyekundu, nahodha Noela Luhala aliyepewa kipindi cha pili.

Huku Zainabu Mohamed (Dudu) aliyepewa kadi hiyo kipindi cha kwanza na kutengeneza rekodi nyingine kwa Tanzania kung’oka kombe la dunia ikiwa timu iliyopewa kadi tatu nyekundu.

Mchezaji wa kwanza alikuwa mshambuliaji Neema Paul, aliyepewa kadi hiyo kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Japan, Tanzania wakipoteza kwa mabao 4-0.

Licha ya kuondolewa kwenye mashindano, benchi la ufundi la timu hiyo limeweza kufikia malengo waliyojiwekea ya kuweza angalau kufika hatua ya robo fainali kutokana na ugeni na uchanga wa kushiriki mashindano hayo.

Ikumbukwe kuwa hii ilikuwa ni mara ya kwanza Tanzania inashiriki mashindano makubwa ya FIFA na walifika hapo kwa kuwatoa vigogo Cameroo.

Serengeti Girls
Serengeti Girls

Serengeti ilitinga hatua ya robo fainali kwa kuwachapa Ufaranasa mabao 2-1, kutoka sare na Canada ya bao 1-1, huku wakifungwa na Japan ambao walikuwa vinara wa kundi D.


Unaweza kua kutazama video za uchambuzi na matukio ya kisoka kwa kugusa video hii

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.