Kocha wa Simba SC, Steve Barker, amesema mechi ya kesho ni muhimu kwa timu zote mbili kwani kila klabu ina nia ya kupambana kupata alama za ligi.
Barker aliongeza: “Azam ni timu nzuri. Wana kocha mwenye uzoefu na wachezaji wazuri, lakini maandalizi yao yanaendelea vizuri.” Nahodha wa Simba, Shomari Kapombe, alisema: “Tumefanya maandalizi mazuri na tutakwenda kucheza mchezo wa kuvutia.”
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa upande wa Azam FC, kocha Florent Ibenge alisema: “Simba sio timu ndogo. Kesho tunakwenda kucheza mechi yenye hadhi ya Afrika kwa sababu timu zote mbili zilishiriki katika hatua ya makundi ya mashindano ya kimataifa.”
Mchezaji wa Azam, Nathaniel Chilambo, aliongeza: “Kama wachezaji tuna nafasi nzuri kuonesha kile ambacho kocha wetu anakitaka.”
Mechi hiyo ya wa Ligi kuu ya NBC, unaojulikana kama Mzizima Dabi, utachezwa kwenye dimba la Azam Complex majira ya saa 1:00 usiku, ambapo mashabiki wanatarajiwa kushuhudia pambano la kihistoria kati ya klabu hizo mbili.

