Jicho la Napoli kwa Umtiti Mbadala wa Koulibaly!

Mlinzi wa Barcelona, Samuel Umtiti ameingia kwenye kipaumbele cha Napoli kama mbadala wa Kalidou Koulibaly ikiwa klabu itamuuza.

Kuna ripoti kibao kuwa Kalidou Koulibaly anataka kusepa Stadio San Paolo msimu huu wa joto, na hivyo tayari klabu nyingi zikiwemo Real Madrid, Manchester United na Paris Saint Germain zimeonesha nia ya kutakla kumsajili.

Bila shaka Napoli wanahitaji mbadala wa kuziba pengo litakalo achwa na Koulibaly, na kwa mujibu wa ripoti Umtiti ndiye nyota pekee ambaye amefikiriwa kupewa kipaumbele zaidi na klabu hii.

Nyota huyu ana miaka 26 na raia wa Ufaransa, alisajiliwa kutokea klabu ya Olympique Lyonnais mwaka 2016 kwa dau la paundi milioni 25. Dau la staa huyu kwa sasa linatajwa kuwa paindi milioni 50.

Hata hivyo inahofiwa kuwa staa huyu anweza kuuzwa kwa dau dogo zaidi kwa sababu ya changamoto ya kiuchumi iliyoletwa na janga la covid19 amabayo imepelekea kushuka kwa ada za wachezaji Ulaya.

Hata hivyo, Umtiti hajawa na msimu mzuri sana mwaka huu baada ya kupata changamoto mara kadhaa za majeraha akiwa amecheza mechi 16 tu msimu huu akiwa na Barcelona.

Man United wanafikiria kuwa Umtiti anaweza kuwa mbadala wa Koulibaly ambaye atawagharibu karibu paundi milioni 100.

2 Komentara

    He should come to the premier league

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.