Klabu ya Juventus imeingia tena kwenye mikono ya sheria baada ya polisi kuanza kuwachunguza viongozi wake wa juu dhidi ya matumizi ya pesa zilizotumika kuuza na kununua wachezaji kati ya 2019 na 2021.
Mwenyekiti Andrea Agnelli, kaimu mwenyekiti, mchezaji wa zamani Pavel Nedved, na msimamizi mkuu wa fedha Stefano Cerrato, na viongozi wengine waandamizi wapo chini ya upelelezi dhidi ya matumizi hayo.

Muendesha mashitaka Anna Maria Loreto, alisema kwenye waraka wake uliotoka siku ya ijumaa kwamba upelelezi huo ni kuthibitisha kama maafisa wa Juventus walitoa taarifa za uongo kwa wawekezaji na kutoa risiti kwa malipo yasikuwepo.
Mwezi septemba, klabu ya Juventus walisema kuwa taasisi ya udhibiti masoko ya Italia “CONSOB”, walikuwa wanawachunguza kwenye mapato waliyopokea kutoka kwenye mauzo ya wachezaji, waendesha mashitaka wa serikali ya Italia mwezi uliopita walianza uchunguzi kuhusu uhamishisho wa baadhi ya wachezaji kwenye serie A.
Wiki nyingine ya kushinda mamilioni ukiwa na kasino maridhawa za meridianbettz. Mchezo pendwa wa Fai Cai Shen unakupa thamani ya dau lako, kwa kiasi kidogo cha dau unaweza kushinda mkwanja mrefu.


