Kisa Kichuya, Simba Wapigwa Faini na FIFA

Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Mwina Kaduguda amesema sakata nyota wao wazamani Shiza kufungiwa miezi sita huku wao wakipigwa faini watalitolea ufafanuzi baada ya Bodi yao kukutana.

Jana kulitoka taarifa kutoka Shirikisho la soka Duniani (FIFA) kumfungia Kichuya miezi sita huku Simba ikipigwa faini ya dola 130,000 ni zaidi ya Shilingi Milioni 300 kwa kuondoka timu ya Pharco ya Misri bila kutoa taarifa kwa uongozi na hakupewa barua ya ruhusa (Release Letter).

Kaduguda amesema Bodi yao yenye watu 17 ikikutana anaamini suala hilo halitakuwa kubwa na amewataka wanachama na wapenzi wa Simba watulie wasubiri maamuzi ya Viongozi.

Kiongozi huyo ameongeza kuwa kwenye sakata hilo huenda wao wakawa hawana kosa lolote hivyo watapeleka utetezi wao na kwa uzoefu wake kila kitu kitakaa sawa.

“Hili suala tumelisikia, tunasubiri Mtendaji wetu mkuu alilete kwenye Bodi lijadiliwe na ni matumaini yetu litamalizika vizuri kwakua tuna watu imara wa kufanya hilo,” amesema Kaduguda.


MALIZA MWAKA KIBINGWA KWA KUJISHINDIA SHEA YAKO KWENYE SHILINGI 140,000,000TSH!!

Kipindi hiki cha sikukuu kinamalizika kwa namna ya kipekee. Shilingi 140,000,000 kushindaniwa katika michezo ya Evolution kwenye Kasino Mubashara ya Meridanbet. Ingia mchezoni na ujiwekee nafasi ya kushinda shea yako!!!

SOMA ZAIDI

16 Komentara

    Hilo ni kosa ya kichuya mwenyewe

    Jibu

    Iyo adhabu ni ya huyo kichuya

    Jibu

    Kichuya ni moto

    Jibu

    Mwenye kosa nikichuya

    Jibu

    Mambo ya adhabu sio poa kabisaa

    Jibu

    Duuh sio powah

    Jibu

    Walipe tu.no way out

    Jibu

    Dhuuu amna jinsi

    Jibu

    Amna namna

    Jibu

    Yupo huyoo

    Jibu

    Kichuya ndio ana makosa

    Jibu

    Duu siyo poa mjanga hayo

    Jibu

    Duu pesa nyingi mbona huyu Kichuya katuletea mambo meusi

    Jibu

    Duh majanga kwl

    Jibu

    Poleni sana wana simbaa maana hilo ni balaa kubwa sana

    Jibu

    Kichuya ameiweka klabu matatani kwa kosa lake

    Jibu

Acha ujumbe