Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp amepata pigo baada ya kufiwa na mama yake mzazi, Elisabeth aliyefariki jana Jumatano, februari 10, 2021.
Jurgen hataweza kuhudhuria mazishi ya mama yake nchini Ujerumani, kutokana na masharti makali yaliyowekwa na Ujerumani katika kupambana na maambukizi ya virusi vya Covid 19.
“Alikuwa ndiyo kila kitu kwangu, alikuwa mama bora sana kwangu, kwa kuwa mimi ni Mkristo, naamini atakuwa sehemu bora peponi, ” amenukuliwa Kocha huyo na kuongeza kwamba maambukizi ya Corona yatakapotulia, amepanga kufanya hafla ya kipekee kumuenzi mama yake huyo.
Elisabeth na mumewe Norbert Klopp aliyefariki mwaka 2000 akiwa na umri wa miaka 66, walifanikiwa kupata watoto watatu, Stefanie, Isolde na Jurgen.
Kupitia akaunti yake ya mtandao wa Twitter, Klabu ya Liverpool imetoa salamu za rambirambi kwa kocha huyo kwa kumsindikiza na maneno ‘You will never walk alone Klopp’ na kusindikizia na alama ya kopa, ukiwa na maana kwamba Klopp hayupo peke yake katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mama yake.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Caroline
Pole Sana Klopp
Magdalena
Klopp pole kwa kipindi kigumu
Sadick
Ni jambo gumu sana kufiwa na Mama yako na kushindwa kuhudhuria mazishi yake. RIP Mama Klopp.
Rahma
Dar pole sana klopp kwa msiba mzito
Lydia Emmanuel Magoti
Daah pole yake kloop
Dorophina
Pole yake klopp pigo kubwa amepata
Adelta
Pole yake klopp
Mama pumzika kwa amani 😭😭
Khadija
Pole sana R.I.P
Sylvester
Pole sana Klop kwa msiba mkubwa uliokukuta
Issa
Pole jurgen pigo sana
Angelina
So sad
Sania
Pole sana Klopp
Mwanahamisi
Pole yake klopp
Neema juma
Pole zimfikie klopp
Sarah
Pole sana klopp
Hopemwaikuka
Polen sana
warda
Pole yake jamani