La Liga Ipo Tayari Na Maisha Bila Messi.

Katika hali ya kawaida, hakuna mchezaji mkubwa kuliko timu na vilevile hakuna timu kubwa kuliko shirikisho la soka la mahali husika. La Liga ipo tayari na maisha bila ya Lionel Messi.

Mapema mwezi Agosti, Lionel Messi aliwasilisha maombi yake ya kutaka kuondoka kwenye klabu ya Barcelona. Mchakato ambao uliteka vichwa vya habari duniani kwa muda kufuatia sakata hili kuwa na maelezo mengi kwa kila upande uliohusika.

Japo ombi la Messi halikufanikiwa na aliendelea kubaki Barcelona, La Liga ilishuhudia raisi wa Barca – Josep Maria Bartomeu akijiuzulu baada ya sakata la Messi kuondoka Barcelona kuisha.

Hii haijawashtua La Liga na wametolea mfano baadhi ya wachezaji waliowahi kuondoka kwenye ligi soka nchini Hispania lakini maisha yameendelea bila tatizo lolote na ushindani upo vilevile.

Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Neymar Jr.

Akizungumza na waandishi wa habari, Raisi wa La Liga – Javier Tebas amenukuliwa akisema “Tungependa Messi abaki lakini Ronaldo na Neymar waliondoka na hatujaona tofauti yoyote mpaka sasa. Tupo tayari.

“Inaonekana timu pekee kwenye Premier League ambayo ilisemekana inamtaka Messi ni Manchester City, hawa wanafanya kazi nje ya utaratibu. Sio mimi tu ninayesema hili.

“Sina uoga wowote dhidi yao. Mara kadhaa nimewakosoa kwa wanachokifanya. Kukirudia tena kwa mara nyingine haina tofauti yeyote. City hawajaathirika na COVID au gonjwa lolote au changamoto yoyote kwa sababu wanamfumo tofauti wa kifedha na ni ngumu kupambana na hilo.”

Je, Messi ataondoka kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu huu au ataamua kusaini mkataba mpya na Barcelona hasa baada ya Bartomeu kujiuzulu na ujio wa uongozi mpya?


BASHIRI UKIWA MAHALI POPOTE!

Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.

Meridianbet Beti Popote

INGIA MCHEZONI!

29 Komentara

    kama laliga wameamua bila messi soka aliwezi kuzuirika basi haina tabu maisha ya soka yaendelee tu

    Jibu

    La liga iko vizuri na inajiamini itazidi kunoga

    Jibu

    Acha maisha ya soka yaendelee na la liga kama kawa kwani Messi yeye nan mpaka akwamishe laliga

    Jibu

    Leo kazi ipo

    Jibu

    La liga ipo vizuri .

    Jibu

    Yuko sahihi

    Jibu

    Ni kauli ya kishujaa. Maisha yanatakiwa kuendelea bila Messi.

    Jibu

    La liga acheni maneno maneno kwani messi ndio amebeba timu au yeye ni mchezaji kama wachezaji wengine mbona mnaleta ushamba au mmeshapewa chenu na Barcelona mnaanza maneno madogo dogo acheni hizo akiamua kuondoka ni yeye mwenyewe na kikosi chake kama ilikuwa hamumtaki si mngemuacha akaondoka mbona mlimuwekaa vikwanzo ni kwa sababu mlikuwa munamuhitaji hasaivi mnaaza kutupigia kelele.

    Jibu

    La liga nao wamuache messi amalizane na Barcelona bila maneno maneno wamuache akamalizie soka lake anapotamani kumalizia

    Jibu

    wamuache akamalizie soka lake anapotamani kumalizia

    Jibu

    Hakuna mchezaji mkubwa kuliko timu

    Jibu

    La liga ipo vizuli

    Jibu

    La liga haishindwi bila mess

    Jibu

    Barcelona kama wana mtaka messi waendelee nae na bishara wamuongezee dau tu pesa ndio kila kitu

    Jibu

    Mmmh laliga nao wanamaneno kama bongo tu

    Jibu

    Jamani kwan Messi kawakosea nn mbona hvyo

    Jibu

    Kauli nzuri sana alilosema na inawezekana kabisa

    Jibu

    La liga mambo ni moto.

    Jibu

    Kumekucha huko laliga

    Jibu

    Mambo yamepamba moto

    Jibu

    Ni kauli ya kishujaa tu ila ukwl ni mwamba La liga bila messi haina mvuto na vile vile wanapotezah pesa nyng Sana kutokuwepo messi ndani ya la liga

    Jibu

    Mmmmmhh naona sio powa kabisa

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    La Liga bila messi inawezekana

    Jibu

    Yuko sahihi

    Jibu

    Mbona hili gumzo tena wamuache aende anapo taka kwenda akamalizie soka lake semu anapo pataka Messi kasha choka kusalia hapo Barcelona wamuache ende tuu

    Jibu

    La liga IPO vizuri

    Jibu

    Asnt kwa taarif meridianbet

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.