La Liga wanaweza kuanza kuwaruhusu mashabiki kuhudhuria dimbani kwenye mechi za wiki nne za mwisho za msimu wa 2020-21.
Mashabiki kwa sasa hawaruhusiwi kuingia uwanjani kuhudhuria mechi kutokana na masharti ya kupambana na korona yanayofuatwa kitaifa na ukanda mzima wa kuepuka mikusanyiko.
Hata hivyo, kwa mujibu wa taarifa toka Hispania, jambo la kuruhusu mashabiki limewekwa mezani, na linafikiliwa ikiwa linaweza kutumika katika wiki za mwisho za mechi za ligi.
Kutokuwepo kwa mashabiki kumeathiri sana sekta ya michezoi, vilabu vikipata mapato machache kuliko awali. Ripoti zinasema kuwa mpango mamlaka za La Liga ambao upo mezani sasa, ni kurejesha mashabiki kuanzia wikiendi ya pili ya mwezi Mei.
Hii inatarajiwa kuhusisha asilimia 25 ya uwezo wa uwanja, na mashabiki wa ugenini hawataruhusiwa. Pia mashabiki watatakiwa kuvaa barakoa na kutosimama au kushangilia kwa umbali wa karibu na wengine.
Kwani Meridianbet Wanasemaje! Mkwanja Upo Kwenye Kasino mpya ya Mini Power Roulette.
Unawezaje kukosa ubingwa ndani ya kasino hii maridhawa, Nafasi ya kushinda mkwanja ni kwa kila mtu, Meridianbet inakupa nafasi ya kuwa mmoja ya washidi leo, unasubiri nini?



Johnmary jo
Itakuwa poa sana tulimisi sana raha mechi kushangiliwa#meridianbett#
Venerose
Safi sana mashabiki wana umuhimu wao
aisha
Kama covid hamna itakua pouwah sa a
dorophina
Nice update
Elika
Asante kwa taarifa
Caroline
Tujifunze kuishi na covid
Issa
Italeta hamasa sana
Sarah
Asante kwa taarifa
neema hassan
Wachukue tahadhari za kutosha
Magdalena
Wawaruhusu tu
Lydia Emmanuel Magoti
Itakuwa poa tuuu
Sania mapua
Mashabiki muhimu ila covid sio poa