Liverpool, 30 Tena! - Roy Keane

Jahazi linaendelea kuzama linapokuja suala la Liverpool kutetea ubingwa wa EPL msimu huu. Hii ni baada ya kupoteza mchezo wa 3 wakiwa Anfield.

Mabingwa wa tetezi wa EPL wamejikuta wakiambulia kipigo kizito cha magoli 4-1 kutoka kwa Manchester City jana usiku.

Mengi yamesemwa baada ya mchezo huu, lakini la Roy Keane limekuwa na maono tofauti. Keane ambaye amekuwa akichambua mienendo ya timu mbalimbali, anaiona Liverpool ikirudi ilipotoka.

“Kwangu ni mabingwa wabaya. Utasema huu ni msimu wa kipekee, ni Corona. Lakini sio sababu, nyie ni mabingwa watetezi, nyie ni Liverpool.

“Endeleeni kucheza hivi na mtakaa miaka mingine 30 bila kombe.” alisema Roy Keane baada ya mchezo dhidi ya City.

Kocha Jurgen Klopp amekuwa ni mwenye kutafuta sababu kwa kila mchezo anaocheza msimu huu. Kwa hali ilivyo sasa hivi, majogoo ya Uingereza yanapungufu ya pointi 27 wakilinganishwa na walivyokuwa muda kama huu msimu uliopita.

Hii ni kusema kuwa Klopp na vijana wake hawana jipya msimu huu au ni wapi hasa wanaelekea?


TENGENEZA MKWANJA UKIWA NA MERIDIANBET 

Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye  kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.

SOMA ZAIDI

16 Komentara

    Liverpool bado wanafuraha ya ubigwa ndo mana wanapoteza sana

    Jibu

    Liverpool msimu huu waandike maumivu

    Jibu

    Livepool msimu huu wameula wa chuya

    Jibu

    Liverpool wanatakiwa wafanye kazi ya ziada

    Jibu

    Liverpool wanakazi nzito wanatakiwa wapambane

    Jibu

    🤣🤣🤣🤣

    Jibu

    Liverpool walikuwa na kibarua kizito sana jana

    Jibu

    Liverpool hawako sawa

    Jibu

    Mpira hasa EPL kumekuwa na changamoto sana maana kila timu imejipanga kisawasawa japokuwa kuna mapungufu madogo madogo, Muda umefika kwa Klopp na vijana wake kujaribu kurudi kwenye mbio za ubingwa, Squard rotation inahusika kwa Liverpool japokuwa kwa upande mwingine ni jambo gumu sana kulifanya kwa wakati ambao unahitaji ushindi

    Jibu

    Liverpool wanayumba

    Jibu

    Liverpool win

    Jibu

    well

    Jibu

    Liverpool hawaii sawa

    Jibu

    Liverpool Wana kwama wapi sasa

    Jibu

    Jamani Liverpool wanatuangusha sana

    Jibu

    Inawezekana ikawa kweli kwani naona wchezaji wengi bora kama Salah wataondoka pale

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.