Liverpool wameripotiwa kuwasiliana na Lazio juu ya uwezekano wa kumchukua kiungo wao Sergej Milinkovic-Savic.
Mchezaji huyo wa miaka 26 alifanya vyema kwenye kampeni ya mwisho kwa upande wa Italia, akifunga na kusaidia jumla ya mabao 17 kwenye Serie A.
Milinkovic-Savic sio mgeni kuhusishwa na uhamisho wa kwenda Ligi Kuu, kwa muda mrefu alikuwa akionekana kuwa kwenye malengo ya Manchester United.

Kwa mujibu wa Calciomercato, Liverpool pia inaonyesha nia ya kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Serbia kabla ya kuanza kwa msimu mpya.
Ripoti hiyo inadai kwamba Liverpool, wamefanya mawasiliano na Lazio ili kujua uwezekano wa kukamilisha biashara ya Milinkovic-Savic.
Hata hivyo, inaripotiwa kuwa upande wa Jurgen Klopp haujajiandaa kutumia pesa nyingi kwa kiungo huyo, ambaye anaaminika kubeba uthamini wa € 70m (£ 60m).
IcyGems kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet. Ndio, ukiwa kwenye nyumba ya mabingwa, ndipo utakapoufurahia ubora wa Kasino ya Mtandaoni sambamba na kushinda kwa ushindi mkubwa! Ishi na hii, IcyGems!


Issa
Wamchukue jembe