Liverpool wameshinda mechi mbili pekee kati ya sita tangu kuanza kwa msimu huu na bado hawajaibuka washindi kwenye mechi zao za ugenini.

Baada ya kulazimishwa sare tasa katika mchezo wa Merseyside dabi dhidi ya Everton, Alisson Becker anasisitiza kuwa Liverpool “wanalenga sana kurudisha ushindi”. Liverpool sasa lazima waelekeze mawazo yao kwenye Ligi ya Mabingwa watakaposafiri kwenda Napoli.
Ulikuwa ni mchezo wa kukaribiana huku walinda mlango wakiwa na ubora wa hali ya juu, kabla ya VAR kufanya jambo kubwa zaidi kwa dakika 20 za mchezo, na kuzima bao la karibu la Conor Coady wa Everton huku beki akiwa ameotea tu, hivyo basi timu hizo kugawana alama moja kila mmoja.

“Tuna malengo sana ya kupata ushindi,” Alisson aliambia tovuti rasmi ya Liverpool FC.
“Ilikuwa muhimu sana kushinda mchezo uliopita dhidi ya Newcastle, sio kila mara unapata matokeo unayotaka lakini lazima upigane kwa hilo, unahitaji kuwa na msimamo katika uchezaji wako, na tunafika hapo. Tunaimarika kwa kuzingatia michezo ya mwisho tuliyokuwa nayo, kila mchezo tunaboresha hatua”“Wachezaji wanarejea kutoka kwenye majeraha kwa hivyo ni muhimu sana na hiyo ndiyo upande mzuri wa kila kitu.”
Alisson, ambaye aliokoa hatari kubwa na kuwanyima magoli Neal Maupay na Dwight McNeil uwanjani Goodison Park, alikubali kwamba Liverpool haikustahili kushinda mchezo huo.


