Miamba wa soka ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL), Liverpool, watakuta na Arsenal kwenye raundi ya 16-bora ya kipute cha Carabao Cup mnamo Oktoba 1, 2020 baada ya kuwakomoa Lincoln 7-2 uwanjani Sincil Bank mnamo Alhamisi.
Arsenal ya kocha Mikel Arteta, ilifuzu kwa hatua ya 16-bora baada ya kuzamisha chombo cha Leicester City kwa mabao 2-0 mnamo Septemba 23 uwanjani King Power.

Wakicheza dhidi ya Lincoln, Liverpool ambao kwa sasa wananolewa na kocha Jurgen Klopp, mabao yao yalifungwa na Takumi Minamino, Curtis Jones, Xherdan Shaqiri, Marko Grujic na Divock Origi.
Tottenham Hotspur walifuzu kwa hatua ya 16-bora bila ya kutoa jasho baada ya kupewa nafasi ya bure. Hatua hiyo ilichangiwa na tukio la idadi kubwa ya wachezaji wa kikosi cha kwanza cha Leyton Orient waliokuwa wavaane na Spurs kuugua Covid-19. Spurs ya mkufunzi Jose Mourinho sasa itachuana na Chelsea ya kocha Frank Lampard.
Chini ya kocha Pep Guardiola, walivaana na Bournemouth na kuwafunga 2-1 kujikatia tiketi ya kuvaana na Burnley katika raundi ijayo ya 16-bora.

Kati ya mechi nyinginezo zilizotandazwa Septemba 24, Aston Villa walipata ushindi wa 3-0 dhidi ya Bristol City uwanjani Ashton Gate na kufuzu kukipiga na Stoke City kwenye mchezo utaoshuhudia mshindi akitinga hatua ya robo-fainali ya Carabao Cup msimu huu.
DROO YA 16-BORA CARABAO CUP:
Tottenham vs Chelsea
Newport County vs Newcastle
Burnley vs Manchester City
Brighton vs Manchester United
Everton vs West Ham
Brentford vs Fulham
Aston Villa vs Stoke City
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.


Hopemwaikuka
Mechi zmetulia Sana kaz kwetu mashabik
Zeiyana
Liverpool wana kutana na viboko wao hii mechi hitakua hapatoshi
Elika
Leo patachimbika hapa
Hidaya
Mshiko nje nje mechi za ushindi
Fatina mfingi
Leo ndio leo!!
Amiri Kayera
Mechi zote kalii
Lydia Emmanuel Magoti
Mechi zote kali patachimbika leo mpaka kiereweke
Mwajumah
Kazi itakuwepo Leo
Nasra
Leo patachimbika
Shan
Ni balaa hapa huku auba kula mane
Gabriel
Natarajia kuona jeshiii la mizinga likifanya yao
# Arsenal jeshiii 🔥🔥🔥
Adelta
Leo Kazi ipo
lombo
mambo ni moto na meridianbet
Rehema
Gemu bomba
aisha
Liverpool kapiga hao kama nawaona watoto wa klopp watavyoitikisa nyavu
Issa
Ni balaa tena arteta ni shida
Ernest
Arsenal sijui wataweka wapi sura zao wiki hii
Sadick
Ndani muda mfupi Arsenal inakutana mara 2 na Liverpool ktk mashindano tofauti na endapo timu mojawapo ikafungwa mara mbili ina maana itakuwa imeonyesha uwezo mkubwa#meridianbettz
Flomena
Good news
Fatuma kasomo
Duh arsenal sijui itakuaje
Janeflora malisa
Mambo mazur
Neema
Leo kutanogaa
Samiah
Leo ndio leo
Latifa juma mohamed
Mechi zote pambe.
David Pere
Natarajia kuona jeshiii la mizinga likifanya yaoh
Sauda
Ratiba imetulia
Caroline
Arsenal jmn.mbona mnatuumiza mashabiki zenu
felister
nina Imani na arsenal msiniangushe ifikapo tar iyo
Rose kapinga
Hatariii wakali wa soka hao!!
Sabrina
Iko poa sana hii
Theckla
Ni mwendo wa kubet na meridianbet
Khadija
Leo kazi ipo
Mnongane JR
Mechi Tami Liverpool vs arsenal
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif
magdalena
wanakutana tena vibonde wa uingereza apo itakuwa balaa tupu
Povel
Don’t miss
Dorophina
Hii mechi itakuwa ngumu sana wamekutana mafahari wawili