Klabu ya Man United imefanikiwa kumalizana na kocha wa kimataifa wa Ureno Ruben Amorim ambaye alikua anaifundisha klabu ya Sporting CP mabingwa wa ligi kuu nchini Ureno ambapo atakua klabuni hapo mpaka 2027.
Baada ya kumfukuza kocha Erik Ten Hag raia wa kimataifa wa Uholanzi siku ya Jumatatu Man United walimpatia timu Ruud Van Nistelrooy aiongoze kwa muda, Huku wakiwa wanatafuta kocha wa kudumu ambapo walifanikiwa kumpata Ruben Amorim kutoka Sporting CP ambapo wamelipa kiasi cha Euro milioni 10 kwajili ya kumpata kocha huyo.Taarifa zinaeleza kocha huyo ataanza majukumu yake rasmi ndani ya klabu hiyo baada ya mapumziko ya mechi za kimataifa mwezi Novemba, Huku mpaka sasa timu ikiwa chini ya kocha Ruud Van Nistelrooy ambaye ataiongoza timu hiyo kwenye michezo minne ambayo ni dhidi ya Leicester City kwenye Carabao ikiwa umeshachezwa, Chelsea, PAOK, na Leicester City kwenye ligi kuu ya Uingereza.
Kocha Amorim anakuja ndani ya Man United pamoja na benchi lake la ufundi ambalo amekua akifanya nalo kazi ndani ya kikosi cha Sporting CP, Huku ikielezwa ndio sababu ya kuchelewa kujiunga na Man United kwakua walikua wanafanya mazungumzo juu benchi la ufundi la kocha huyo na hatakua kwenye benchi la klabu hiyo kwenye mchezo dhidi ya Chelsea wikiendi hii kama taarifa zilivyoeleza awali.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.