Manchester United Yamvalia Njuga Zirkzee

Klabu ya Manchester United inaelezwa iko kwenye mipango ya kumsajili mshambhuliaji wa klabu ya Bologna raia wa kimataifa wa Uholanzi Joshua Zirkzee.

Joshua Zirkzee amekua akifuatiliwa kwa karibu na Manchester United ikiwa inaelezwa anaweza kua usajili wa kwanza kwa Mashetani wekundu katika dirisha hili kubwa, Huku klabu hiyo ikiwa na ushindani mkubwa na klabu ya soka ya Ac Milan kutoka nchini Italia.manchester unitedKlabu ya Ac Milan inaelezwa ilikua karibu zaidi kumsajili mshambuliaji Joshua Zirkzee kutoka Bologna na maslahi binafsi baina ya pande hizo yalishakubaliwa, Lakini Man United wanaonekana kama wanaweza kupindua meza kwakua wako tayari kutoa kiasi husika kinachohitajika.

Klabu ya Manchester United wanaelezwa wako tayari kulipa kiasi cha £34 milioni ambacho ndio kiasi ambacho klabu ya Bologna iliweka kwenye mkataba kama timu yeyote itamuhitaji itapaswa kulipa, Huku United wakiwa tayari kulipa kiasi hicho ni kipindi ambacho Ac Milan walionekana kusuasua kulipa kiasi hicho.manchester unitedSehemu nyingine ambayo klabu ya Manchester United wameonekana kuipiga bao mpaka sasa Ac Milan ni kwa wakala wa mshambuliaji huyo, Ambapo Man United wamekubali kulipa kamisheni ya mauzo ya mchezaji kwa wakala huyo jambo ambalo litarahisisha Mashetani wekundu kumpata mchezaji huyo.

Acha ujumbe