Mason Mount Kukipiga Leo Dhidi ya Palace

Kiungo wa klabu ya Manchester United raia wa kimataifa wa Uingereza Mason Mount anatarajiwa kukipiga leo katika mchezo wa kombe la Carabao dhidi ya klabu ya Crystal Palace.

Mason Mount ambaye amekua nje ya uwanja kwa takribani wiki tatu sasa kutokana na majeraha ana asilimia kubwa za kucheza mchezo wa leo dhidi ya klabu ya Crystal Palace na anatarajiwa kuanza mchezo huo.mason mountKiungo huyo bado hajafanikiwa kuonesha cheche ndani ya klabu hiyo tangu atue klabuni hapo dirisha kubwa lililopita, Lakini mchezaji huyo anatazamiwa kufanya makubwa ndani ya klabu hiyo kutokana na ubora ambao alikua anauonesha ndani ya Chelsea.

Manchester United haijafanikiwa kuanza vizuri msimu ndani ya ligi kuu ya Uingereza na ligi ya mabingwa ulaya, Lakini sababu mojawapo ya sababu ya kutokufanya vizuri kwa klabu hiyo ni majeraha ambayo yanawaandama wachezaji wake akiwemo na kiungo huyo wa kimataifa wa Uingereza.mason mountKiungo Mason Mount anatazamiwa kama mchezaji muhimu wa klabu hiyo kwa siku zijazo, Kwnai kusajiliwa kama usajili wa kwanza kabisa klabuni hapo dirisha lililopita ilitoa taswira kua ni mchezaji wa aina gani Man United wamemsajili na leo rasmi anarejea kwenye kikosi cha timu hiyo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.