Nyota Lionel Messi amekataa taarifa zinazomuhusisha na klabu ya Inter Milan, na kudai kuwa hana mpango huo.
Nyota huyu alianza kuhusishwa na klabu hiyo ya Inter baada ya raisi wa zamani wa klabu hiyo kusema kuwa ndoto ya Inter kumpata Messi inawezekana. Messi pia alikuwa anahusishwa na klabu yake ya zamani ya Old Boys ya Argentina.
Messi amezungumzia taarifa zote mbili ya kuhusishwa na klabu ya Inter Milan na Old Boys. Amesema taarifa hizo zote ni za uwongo, na anashukuru mashabiki wake wake hawaamini taarifa hizo.
Messi alibainisha kuwa kumekuwa na wimbi kubwa la kuongezeka kwa taarifa za uongo kuhusu hatma yake klabuni Barcelona. Licha ya taarifa kuwa alikuwa na mvutano na viongozi wa Barca lakini Sky Sport waliripoti kuwa ana mpango wa klabuni hapo.
Taarifa zinataja kuwa klabu ya Barcelona inatarajia kukaa mezani na staa huyu ili kufikia maridhiano ya kuongeza mkataba wa Lionel Messi kwa miezi ijayo, lakini hali ya sasa ya uchumi inatia wasi wasi kulingana na Janga la virusi vya corona.


Amani
Anajua atapoteza mvuto ndo maana ataki messi wa baka tu
Asha mvugalo
Huyu messi kanywa maji ya Barca.
Ester jackson
Lion messi anaangalia masilahi sana ameona kuwa huko hatakuwa zaidi na pia hata akibaki Barcelona bado yutabaki kuwa mashabiki wake