Milan Yatwaa Scudetto Baada ya Miaka 11.

Kwa mara ya kwanza tangu msimu wa 2010-11, AC Milan wametawazwa mabingwa wa Italia msimu wa 2021-22, baada ya vita kali ya kutwaa Scudetto dhidi ya wapinzani wao Inter.

Ulikuwa muongo wa kudhalilishwa kwa Milan, wakati Juventus wakishinda taji hilo mara tisa kabla ya Inter kutwaa na kupunguza ukame wa taji hilo msimu uliopita.

 

Dakika ya 17, Olivier Giroud alianza kufunga kwa bao lake la 10 la ligi msimu huu na haikuchukua muda akaongeza la pili dakika ya 32. Dakika nne baadaye, Franck Kessie aliendeleza uongozi wa Milan hadi 3-0, na kuihakikishia timu yake ubingwa.

Milan imekuwa katika kiwango bora tagu mwishoni mwa Januari, wakicheza mechi 16 bila kupoteza kwenye ligi tangu walipofungwa na Spezia Januari 17 na kuruhusu mabao sita pekee katika kipindi hicho.

Ibrahimović alikuwa sehemu ya timu hiyo ikitwaa taji la mwisho, alipochukua nafasi ya mfungaji bora wakati akiwa kwa mkopo kutoka Barcelona, na alikuja tayari kusherehekea baada ya kunyakua taji.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe