Mchezaji Memphis Depay na klabu yake ya soka ya Olympique Lyonnais wapo katika muendelezo wa mazungumzo ya kumfanya Mholanzi huyo aongeze mkataba klabuni kwake.
Rais wa klabu hiyo ya ligi kuu ya nchini Ufaransa, Jean-Michel Aulas ameyasema hayo.
Depay alipewa kitambaa cha unahodha kutoka kwa kocha Rudi Garcia kufuatia kuondoka kwa Sylvinho mapema wakati wa msimu wa mwaka 2019-20 na amefunga jumla ya magoli nane kwenye ligi akiwa amecheza mechi 13 pekee kabla hajakumbana na majeraha ya goti kwenye mechi waliyokula kichapo cha 1-0 walipokutana na Rennes mwezi Desemba mwaka jana.
Mchezaji huyo wa zamani wa klabu ya PSV Eindhoven ambaye amekuwa na klabu ya Lyon tangu alipotokea kwa Mashetani Wekundu, Manchester United mwezi Januari mwaka 2017, amesaliwa na mwaka mmoja pekee katika mkataba wake wa sasa dimbani Groupama, lakini OL wanataka waendelee kuwa naye kwa muda mrefu zaidi.
“Lengo lake lilikuwa ni kucheza EURO, ambayo imeahirishwa kwa sasa,| alisema hayo Aulas. Alitaka sana kucheza kwenye hatua ya 16 bora ya michuano ya Champions League katika mechi za pili dhidi ya klabu ya soka ya Italia, Juventus, ambayo ilihairishwa pia pamoja na ile ya fainali ya Coupe de la Ligue BKT. Anajiandaa kuwa tayari kwa hilo.
“Siku zote nimekuwa na mahusiano ya moja kwa moja na mchezaji huyo. Siku zote amekuwa akiniambia kuwa endapo tutakuwa na makubaliano mazuri ya kikazi basi yeye hana shida na suala la kuongeza mkataba wake na atakuwa tayari kufanya hivyo.”
Depay, mwenye umri wa miaka 26, amefunga jumla ya mabao 43 na kusaidia mengine yapatayo 33 katika mechi 102 za Ligue 1 kwa klabu ya soka ya Olympique Lyonnais na amefunga mara sita na kusaidia upatikanaji wa mabao manne kwenye mechi 13 za michuano ya UEFA Champions League kwa klabu hiyo ya Ufaransa.


mwakalosi
depay ni bonge la mchezaji tatizo anataka kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja akeshe studio then asubui aende mazoezini ila kwa vile ligi ya ufaransa ni nyepesi anaweza kuimudu
Elika
Ni vizuri wamuongezee mkataba ili aendelee kubaki hapo
Juliana
Gud news kwake,aongeze tu mkataba maana umri wake bado upo fit
aisha
Depay yuko vizuri aongezwe mkataba aendelee kufanya kazi
Mariam mtandama
Asante meridianbet #kwa taarifa
Tahiya
Anastahili kuongezewa mkataba ana rekodi nzur
Mwanaidi
Ni mchezaji mzuri lakini ni ngumu kufanya vitu viwili kwa wakati mmoja aache tamaa
Neema hassan
Depay mchezaji mahiri sana tatizo hawezi kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja…
Devotha
Depay ni mchezaji mzuri
dorophina
Ni mchezaji mzuri lakini anataka mambo mengi kwa wakati mmoja
winfrida
depay amefunga magoli zaidi ya nane kwenye ligi akiwa amecheza mechi 13 so ni mchezaji mzuri
Samiah
Depay nimchezaji mahiri
Ester jackson
Lengo lake lilikuwa ni kucheza EURO, ambayo imeahirishwa kwa sasa#meridianbettz
Rehema Dickson
tatizo anataka kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja akeshe studio then asubui aende mazoezini ila kwa vile ligi ya ufaransa ni nyepesi anaweza
Rehema
Depay Ni mchezaji mzuri asiependa makuu
Warda
Olympique wanampenda sana Depay#Meridianbettz
Hope mwaikuka
best prayer ever
Agness
Depay ni mchezaji mzuri Sana
Antony Luseno
Lyon wana kila sababu ya kumbakisha huyu Depay maana kadhiririsha kiwango chake
Aziza mushi
Delay ni mchezaji mzuri tatizo Sasa hawezi fanya Mambo mawili kwa wakati mmoja.
David pere
Kwa kiwango chake Lyon timu inayomfaaa aendelee kukipiga pale
Neema juma
Katisha kijana Depay yuko vizuri mno
Hamidu
Depay fundi wa Mpira ..Kama ataongezA mkataba atakuwa amefanya wazo zuri sana
Asha
Depay mchezaj mzur wa muongezeh mkataba tu
felister
mshika mawili moja mponyoka
Ernest
Depay fundi sanaaaa
Frank Patrick
wampe mkataba fundi bishoo
Gabriel
Kwa upande wng inabid aangalie msalai kabla ya mkataba
Shafii
Depay kwa Sasa yuko kwenye form
Emmy cleopa
Depay yuko vizur sana
Povel
Depay yupo vzr sana wamwongeze Mkataba tu
Amani
depay ni bonge la mchezaji tatizo anataka kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja music na mpira atulie asakate kabumbu
Magdalena
Kulingana na record yake kuwa nzuri anastahili kuongezewa mkataba
Mwajuma
Kama wakimuongezea mkataba watakuwa wamefanya jambo la busara.
Theonestina
Namkubar Sana Depay
Kenani
Itakua poa sana
Zeiyana
Shika mbili moja uponyoka tu
Salma
Yupo vizuri anastahili ilo
Theckla
Apewe mkataba tu
Isaya massawe
Ana rekodi nzuri sana
#meridianbettz
Ester mmakasa
Mbona anafanya vizuri kwa nafasi yake apewe uwo mkataba.
Johnmary joel
Depay ninamkubali sanaa#meridianbetz
Furahav
Yuko vizuri kija