Mchezaji Mustafi anaamini kuwa ni muhimu sana kuwa na mtazamo chanya juu ya kila kitu maishani.
Ikiwa ni sehemu ya program ya Mental Heath Awareness Week, mlinzi wa klabu ya Washika Mitutu wa London, Arsenal, Shkodran Mustafi aliongelea suala la utu wema na kuwa na mtazamo mwema juu ya kila jambo maishani.
Mlinzi huyo wa Arsenal alijadili juu ya kuepukana na mawazo mabaya maishani na umuhimu wa kutendeana mema wakati wa janga la Corona.
Program ya Mental Health Awareness Week ilifanyika mnamo tarehe 18 hadi tarehe 24 ya mwezi Mei ambapo wachezaji kadhaa wa klabu za soka za Premier League walielezea afya zao za akili.
Kuendelea kuwa na maono sahihi wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa Corona ilikuwa ni jambo gumu sana lakini mwanakabumbu wa Arsenal anaamini kwamba unapoamua kuwa na maono chanya juu ya masuala mbalimbali iansaidia sana kukuokoa na matatizo ambayo huenda yangekupata.
“Madaktari wote wanafanya kazi nzuri sana na sisi kama taifa tunajitahidi kupambana na hali hii ila kitu cha muhimu ni sisi kuwa na maono chanya juu ya kila kitu,” alisema hayo Mustafi.
“Endapo tungeweza kuwa na mtazamo chanya juu ya mambo mbalimbali basi tungepata urahisi sana wa kutatua matatizo yetu ya kila siku na kuwa katika hali nzuri sana maishani hasa kifikra na kiafya. Ila ukishikilia kuangalia tu masuala mabaya na mtazamo mbaya utabakia na huzuni muda wote na kuathiri afya zetu.”
Dhamira ya mwaka huu kwenye Mental Health Awareness Week ni kusisitiza upendo na utu wema miongoni mwetu na mwezi uliopita Mustafi alichangia vyakula kwa watu wapatao 16,000 wakati wa kusherehekea siku ya kuzaliwa huko Islington.
“Kwa kawaida siku ya kukumbuka kuzaliwa unapewa zawadi na unakuwa unazungumziwa wewe siku nzma lakini kwa sababu sikuweza kuwa na familia yangu na marafiki zangu na kila mtu awaye yote, nikawaza na kujiambia kuwa ni muda muafaka wa mimi kutoa badala ya kupokea,” alisema.
“Hasa wakati huu ambapo hali ni mbaya na tunapitia magumu maishani, tunatakiwa kujitahidi kusaidiana kwa hali na mali, kufanya yale tunayotaka kufanyiwa na tutaishinda vita hii pamoja.”


Shafii
Yuko sahihi sikuzote mafanikio yanakuja kwa ushirikiano
Antony Luseno
Mustafi katisha sana kwa wazo lake
Salma
Nkweli kabsa yupo sahihi umoja ni nguvu
Warda
Mustafi tokea nimjue leo ndo kaongea point#Meridianbettz
Neema hassan
Mustafi anastahl kuwa mfano wa kuigwa kwa jamii..
Zeiyana
Safi sana mustafi mungu akujalie moyo huo huo
Hope mwaikuka
True 🙊
Mwanaidi
Ni jambo zuri alilosema Shkodran Mustafi kuwa na umoja wa kutatua matatizo ni suala la utu wema na mtazamo mwema maishani
David pere
Wakiamua wataweza kutatua matatizo ya lakini wanatakiwa wajipange sanaa
Rehema Dickson
Kwel kwenye ushirikiano kuna mafanikio
Theckla
Hajakosea
aisha
Sawa mustafa kweli umoja ni nguvu
Christopher
Kweli, ni muhim kufanya kazi kama team
Ester jackson
Hasa wakati huu ambapo hali ni mbaya na tunapitia magumu maishani, tunatakiwa kujitahidi kusaidiana kwa hali na mali, kufanya yale tunayotaka kufanyiwa na tutaishinda vita##meridianbettz
Evaluziga
Nikweli kabisa umoja ni nguvu
winfrida
umuhimu wa kutendeana mema wakati wa janga la Corona.ni mawazo mazur aliyo amua pia ni beki mzuri#meridianbettz
felister
safi
Ester mmakasa
Hajakosea kabisa na wazo lake .
Aziza mushi
Asanteni kwa habari meridianbet.
Caroline
Ni mawazo mazuri..
amani
Hasa wakati huu ambapo hali ni mbaya na tunapitia magumu maishani, tunatakiwa kujitahidi kusaidiana kwa hali na mali kuepukana na huu ugonjwa wa corona na mambo mengine yaendelee
Magdalena
Mustafi yupo sahihi umoja n nguvu
Genia Sikaluzwe
Hajakosea ni wazo zuri
Gabriel
Mental Health Awareness Week inaonekana ni system nzur sana na alichokiongea mustafi yuko sahihi kabisa
Lydia Emmanuel Magoti
Mustafi katisha kwawazo lake akilinyingi huyo
dorophina
Ni vizuri kufanya kazi kwa pamoja
Povel
Yupo sahh anarudish fadhilah kwa jamiii thanks meridian kwa update
Emmy cleopa
Ni vizur sana kufanya kazi kwa ushilikiano
Mwajuma
Mustafi ni beki mzuri sana na anafanya maana huo ushauri wake ni mzuri sana
mathayo sonje
Kuendelea kuwa na maono sahihi wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa Corona ilikuwa ni jambo gumu sana lakini mwanakabumbu wa Arsenal anaamini kwamba unapoamua kuwa na maono chanya juu ya masuala mbalimbali iansaidia sana kukuokoa na matatizo ambayo huenda yangekupata.
Kenani
Ni kwel kabisa ushirikiano ni nguvu
Ernest
Mustafi ameonyesha mfano wa kuigwa sana hasa wa wachezaji wakongwe kama yeye.
mwakalosi
nothing can beat team work haijalishi mko katika hali gani
Tahiya
Yuko sahihi kabisa kusaidiana ni jambo jema hasa katika kipindi iki kigumu tupitacho na ili janga la corona
Devotha
Yupo sawa! Ni kweli wakiungana kwa pamoja wataweza kutatua changamoto zinazo wakabili
Rehema
Yuko sawa anarudisha fadhilah kwa huma
Mariam mtandama
Niwazo mzur
winfrida
mustaphi umeongea maneno mazuri sana endelea kuwa na moyo huo huo
Juliana
Niwazo zuri
Sadick
Bob Marley alisema mkono unatoa ni bora kuliko unaopokea! Mustafa amenena vema na kutenda sawa na maneno yake#meridianbettz
Agness
Yuko sahihi
Hamidu
Mashabiki wa arsenal . Mpo!?nanyie toeni mtazamo wenu
Asha
Kutoa ni moyo Wala si utajir pongez kwake
Khadija
Mustafi yupo sahihi sana#meridianbettz
Samiah
Yuko sahihi
Neema juma
Kazungumza maneno yenye nguvu na wosia ndani yake
Frank Patrick
Busara sana hii
Theonestina
Nice