“Uzuri wa sura ulikuwa aula kweli, lakini ulikuwa si ufunguo wa kila kheri, ubaya wa sura ulikuwa dhila si uongo lakini ulikuwa si zuio la maendeleo, watu waliishi duniani kwa matendo yao siyo kwa sura zao, matendo ndiyo yaliyowatukuza au yaliwadunisha”. Shabaan Robert.
Nimemnukuu Mwanafasihi Hayati Shaban Robert, fumbua fumbo utalewa nini namaanisha! Wakati nakaa kijiweni wazee wangu na Mababu walikuwa wanataja sana jina la Salum Kabunda Ninja sikuwahi kumuona, walitaja jina la George Magere Masatu sikuwahi muona.
Waliniacha zaidi na zaidi waliponitajia Franco Baressi, Martin Kewon, Jaap Staam, Tony Adams bado nilikuwa gizani sana, kila wakitaja majina haya walikuwa wanasikitika sana, walibaki kujisemea dunia hii haina mabeki tena, dunia hii ina watoto laini sana.
Utasema dunia ina beki kama Salum Kabunda alikuwa anachukua mpira mdomoni mwa straika bila faulo?? Utasema dunia ina mabeki wakati Masatu anakuja kukukaba unasikia vishindo kama tembo?? Utasema dunia ina mabeki kama Jaap Stam sehemu ya mguu ataweka kichwa??
Watawezea wapi hawa vijana leo hii straika akifinya beki yupo chini, wangeweza kuendana na kasi ya Ronaldo de Lima?? Wangeweza kumzuia vipi Diego Maradona?? Dunia yenu haina mabeki hii tena, unamkumbuka Daniel Passarella,Allesandro Costacurta au Giacinto Faccheti??
Katikati ya stori zao wakamtaja Nemanja Vidic, hapo nikakaa vyema kwakuwa nimemuona huyu, Babu mmoja alisema Ulaya Mashariki napo kuna mabeki wakatili, Vidic kaishi kwenye moshi wa mabomu na anacheza mpira pembeni ya mizoga, si ajabu yeye kuwa mkatili, ni mtu haswaa.
Katikati ya maongezi wakamtaja Kelvin Yondan, walidai kuna kijana nchini anaitwa Vidic, hapo nilitamani kuwaambia Vidic yule hayupo tena kwa Young Africans, nilitaka kuwaambia kuwa Vidic ameondoka pale, ila kwenye mazungumzo yao walianza kupasifia Mwanza kuwa wana historia ya kutoa vitasa nchini.
Kijana mmoja mfupi sana, umbo dogo sana ambaye kwa macho unaona hasumbui, kwa hisia unaona ni uchochoro ila hiki ni kisiki, mtaani wanamuita Cotton, historia yangu inaanzia mbali sana jioni moja Kelvin Yondan na jezi ya Taifa.
Itaendelea….
Sasa unaweza kuweka pesa moja kwa moja kwenye akunti yako ya Meridianbet kwa kutumia mtandao wa Airtel. Usipate wasi wasi, tunaifanya kazi kuwa rahisi zaidi!


lombo
mambo ni moto na meridianbet
Fatuma kasomo
Gud news
Angelina
Duuh hatari
Neema
Habari imeeleweka
Issa
Yondan skils za kufa mtu uhodar mkubwa hakuna beki kam huyu kutokea vpl
Hopemwaikuka
Kumbe yupo huyu kiumbe
Povel
Bye bye kelvin YOndani (COTTON) umri bado unatak ila mwili tatiz bye bye COTTON taifa stars itakumic Sana na wazee wa kkoo watakumisi sana
David Pere
Yondan skils za kufa mtu uhodar mkubwa hakuna beki kam huyu kutokea vpl
magdalena
yondani yupo makini sana awapo uwanjani ngoja nisubiri mwendelezo kuyajua zaidi kuhusu uyu nyota
Adelta
Yondan akiwa uwanjani anakuwa makini
Ernest
Inashangaza sana, Soka la bongo halina heshima
Caroline
Duhhhhh hii kali sasa
Venerose
Mmh kazi ipo
Lydia Emmanuel Magoti
Yondani nibek mzuri Sana anaejua kujituma kupambana nakuweka mchezo kwenye levo yake Sasa ngoja tuone kinacho jili tusikie mengi kwanyota huyo
Zeiyana
Tunawaombea kila la kheri wapambanaji wetu kila kitu kinaenda na wakati ule ulikua wakati wa (ottoni)yondani na wengine watatokea pia
Tatu
Yondani ni mchezaji mzuri tatizo yanga sijui wanakwama wapi
Janeflora malisa
Kwel kbs muhim umakin
Rehema
Kazi ipo hapo
Mariam mtandama
Duuuh
Sadick
Tatizo la Yondani akishapitwa na mshambuliaji lazima acheze rafu #meridianbettz
felister
duh
aisha
Namkubali sana pia hanaga kazi mbovu
Fatuma kasomo
Mh nomaa
Nasra
Noma sana
Amiri Kayera
History yake Nd ilipoishia ana mpila sasa
Shani
Yondan yanga ilimuach tu lakin ameondoka na mpira wake
Hidaya
Kaondoka na mpira wake
Sabrina
Mambo hayoo!
Saupha mohamed
Yondan mbn yupo vizuri
Sauda
Yondan anajitahidi sana
Gabriel
hakuna beki kam huyu kutokea
Fatina
Yondani Ni mchezaji mzur ila lazima angalie maslai yake upandd mwingine
Mwajumah
Duuh kazi ipo apo
Rose kapinga
Kipaji ichoo