Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema kuwa amemiss sana soka na anatamani kurejea ili aone kikosi chake kikiendelea kufanya makubwa baada ya likizo ya lazima ya Corona.
Klopp anasema atakuwa na furaha isiyo kifani akiwashuhudia Liverpool wakirejea tena dimbani. Kwa sasa klabu za EPL zipo kwenye maandalizi ya kurejea Juni 17.
Liverpool wapo kileleni kwa ponti 25 zaidi, wakiwa wanafukuzia taji lao la kwanza kwa miaka 30 sasa. Bila shaka hii ni nafasi ambayo Liverpool hawahitaji kabisa kuipoteza.
Kulikuwa na wasiwasi ikiwa janga hili la Corona lingekwamisha jitihada walizozionesha Liverpool kutwaa ubingwa kwa namna yeyote. Kuendelea kwa ligi ni tumaini kwao.
Kama ilivyo kwa wapenzi wengine wa soka, wakati huko kimara na mwenge wakisema wana “Mzuka wa kurejea” kwa ligi, Klopp yeye anakwambia “”I have missed it so much it’s unbelievable”, akimaanisha amekumbuka kuwepo dimbani balaa!
Tazama mizuka ya Klopp anapokuwa dimbani, ameikumbuka sana furaha hii 👇
Hata hivyo, Klop amesema bado kuna kazi kubwa sana ya kuifanya wakati Liverpool wakihitaji kushinda mechi nyingi zaidi kadri inavyowezekana ili kujiweka kwenye uhakika zaidi wa kutwaa taji hili msimu huu.
Baada ya kutwaa Ubingwa wa Ulaya mwaka jana, sasa ni wakati wa kutwaa taji la ligi, na kwa mujibu wa meneja huyu ni kuwa hakutakuwa na uafadhali wa nyumbani, mechi zote zitapewa uzito sawa.
EPL imesalia na mechi 92 na mechi zote zinatarajiwa kuwa ziatakuwa zinachezwa bila mashabiki na wachezaji watakiwa kupimwa kila baada ya wiki mbili.


winfrida
habari nzuri kwetu sisi mashabiki ata sisi tumekumisi sana kukuona jurgen
Juliana
Kweli kila wapenda soka tulimiss kabumbu
Ester mmakasa
Me naiyombea Liverpool ichukue hata ubingwa kwa mwaka huu.
Salma
Tuliishia vizuri sisi mashabiki Wa Liverpool tunasubiri kwa hamu muendelezo
Devotha
Mashabiki wako tumekumisi pia
Rehema Dickson
anatamani kurejea ili aone kikosi chake kikiendelea kufanya makubwa baada ya likizo ya lazima ya Corona.
Hope mwaikuka
Vile Yuko na hamu sasa na hii ktu
Mwanaidi
Ni kweli lazima amiss soka na hata sisi mashabiki pia tumemiss soka ile mbayaaa
Evaluziga
Ni habari nzuri kwetu mashabiki wako tumekumis pia
Mariam mtandama
Habari mjema
Neema hassan
Wapenzi wa liverpool tunasubr kwa hamu..
Antony Luseno
Sio kwa klopp tu kila mdau wa soka ana hamu ya kuona mwendelezo wa ligi mbali mbali
felister
ameikumbuka mizuka yake pindi anapokua dimbani
Ester jackson
Tulikuwa na wasiwasi ikiwa janga hili la Corona lingekwamisha jitihada walizozionesha Liverpool kutwaa ubingwa kwa namna yeyote. Kuendelea kwa ligi ni tumain la kweli tu
Neema juma
Nimefurahi kusikia mambo yanarudii siku si nyingi. Tumemic sana
Adelta
Sisi mashabiki tumemisi Sana kumwona
Jurgen klopp akiwa uwanjani
Samiah
Tumemisi sana kumuona Klopp
aisha
Makala safi ila wote tupo pamoja jurgen klopp
Warda
Hata mie nimemic kwa Kweli #Meridianbettz
Theckla
Nami natamani kuona Liverpool ikichukuwa ubingwa
Isaya massawe
Wengi tumemisi soka jamani tunasubir kwa ham sana
Furahav
Wote tumemisi soka,ili tushuhudie liver inavyobeba kombe baada ya miaka 30.
Emmy cleopa
Habar njema
Frank Patrick
Epl panapo hali shwari sina shaka na kulibeba Liverpool ….ninachokisubiri kwa hamu ni Kuwaona ELLIOT,WILLSON,Curtis jones,grujic wakipewa nafasi zaidi na kuwa world class players pale Liverpool chini ya KLOPP….YNWA
Elika
Msimu huu inaimani majogoo ya mji yatachukuwa ubingwa
Shafii
Klop hana lolote anachekelea ubingwaa tu wa EPL
Christopher
Soka ndo linarudi hilo jurgen, soon tu tunaingia uwanjan
David pere
Huyu kocha no chizi wa soka so mchezo Ndio maana anaona Kama ligi inachelewa kurudi
Lydia Emmanuel Magoti
Safii tulikuwa tunasubili kwahamu Mambo mazuri tumemic Sana nasisi
Asia Abdy
Klopp hua ana mizuka sn uwanjan.. namkubal
amani
Baada ya kutwaa Ubingwa wa Ulaya mwaka jana now ana angalia ubingwa wa epl ili kutoa gundu la mda mrefu
Caroline
Tuendelee kuomba.. Mungu atafanya njia
Magdalena
Amesema Jambo la kweli Liverpool watazidi kufanya mambo makubwa
Aziza mushi
Ata Mimi nilimis Sana soka na kumwona klopp.
Zeiyana
Daaah…! Nimic kumuona mo Sarah akiwa dimbani kwa mala yengine tena
Gabriel
Jurgen klopp kocha anamachachali sana
Povel
Ianze tu wakipgeh tumemic hta mashabiki
dorophina
Mashabiki wa Liverpool tunaungana na ww tunasubiria kwa hamu
Mwajuma
Kocha wa soka anatarajia kufanya mambo makubwa sana pale EPL
Kenani
Mpira una burdani moja tam Sana na ambayo mtu huwwz kuisahau na matokeo ya kusisimua
Mwanahamisi
Ianze tuu maana mashabikitumeimis
Ernest
Klop anatuzuga tuu anataka ligi irudi ili akabidhiwe kombe lake wafanye sherehe.
mwakalosi
hata sisi tumemiss vituko vyake ila huyu kuna siku atampiga mtu ngumi maana ana mchecheto sana klopp
Hamidu
Tumemiss vituko vyake klopp
Liverpool watachukua ubingwa baada ya miaka 30 kupita#meridianbettz
Tahiya
Kuwa mkwer mzee baba sema tyuu umemiss kunyakua kombe
Rehema
Klopp tumekumis hatari hatari kuona bwebwe zake
Agness
Nikweli kabisa tumimic Sana soka
Theonestina
Tumemic Sana kwakwer