Pep Guardiola amefuta mkutano wake na waandishi wa habari mchana wa leo wakati akisubili majibu ya uviko-19 baada ya kufanya kipimo cha “Polymerase Chain Reaction” PCR.
Guardiola anaweza kukosa michezo miwili ikiwa atapatikana na ugonjwa, michezo atakayoikosa ni mchezo dhidi ya Newcastle United ambao utachezwa siku ya Jumapili kwenye dimba la St. James’ Park na ambao watawakaribisha Leicester City kwenye dimba la Etihad.

Guardiola ambaye alimpoteza mama yake mwaka jana kutokana na ugonjwa wa Uviko-19, mara ya mwisho kuoneka kwenye mkusanyiko ni kwenye hafla ya kumuaga Sergio Aguero akiiwakilisha timu ya Man City jijini Barcelona.
mkufununzi wa Man City Pep amekuwa akihamasisha watu kuweza kuchukua tahadhari, sio tu wachezaji wake bali jamii kwa ujumla, City wanaenda kwenye mchezo wao wa jumapili wakiwa wanaongoza kwa pointi moja kwenye msimamo wa ligi kuu ya uingereza.
Fanya wiki yako iwe ya ushindi mkubwa ndani ya kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo wa BURST THE BANK🔥🤑 ni moja kati ya mchezo pendwa unaowapa wachezaji mamilioni kila siku. Kwa dau dogo unashinda zaidi.


