Klabu ya AS Monaco imemtangaza Philippe Clement kuwa kocha mpya wa klabu hiyo na kumsainisha mktaba wa miaka mitatu kuchukua mikoba ya Nico Kovac ambaye alifungashiwa vilago.
Philippe Clement ambaye alikuwa kocha wa klabu ya Club Brugge kuanzia mwaka 2019 ameingoza kwenye michezo 129 huku akishinda 71 kutoa sare michezo 33 na kapoteza michezo 25.

Philippe Clement ameisaidia klabu ya Club Brugge kuweza kuchukua ubingwa wa ligi ya Belgium mara tatu mfulululizo huku akiongoza kwenye michezo 40 ya ulaya, pia amefanikiwa kuchukua tuzo mbalimbali akiwa na timu ya Club Brugge ambapo alichukua tuzo ya kocha bora wa mwaka 2018/19 kocha bora wa Ubelgiji 2019/20.
Pia alishawai kchezea timu kadhaa kabla ya kutundika daluga na kuwa mkufunzi, klabu alizowai kuchezea ni Beerschot, Genk, Coventry, Club Brugge na Germinal Beerschot.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


