Mlinda mlango wa Marekani, Gabriel Slonina atajwa moja ya nyota kinda anaewaniwa na Mabingwa wa Ulaya, Real Madrid na Chelsea.
Slonina anayechezea timu ya MLS ya Chicago Fire, ni mchezaji wa kimataifa wa U-20 wa Marekani na ameibuka kuwa moja ya mchezaji bora wa michuano hiyo.
Chelsea na Wolverhampton ni miongoni mwa klabu zilizofanya mazungumzo na Gaga Slonina, lakini ameweka wazi kuwa anataka kujiunga na Real Madrid.
“Huwezi kukataa Real Madrid,” alisema wakala wa mchezji huyo, Garcia.
Klabu ya Chicago Fire ilikataa ofa ya awali ya Golikipa wa Marekani huku wakihitaji dau kubwa zaidi kumuachia kinda huyo.
Chicago Fire wakitarajia ofa nyingine kutoka kwa Madrid. Slonina anachukuliwa kuwa miongoni mwa vijana bora zaidi wa GK duniani.
“Tuna matumaini Chicago watafikia makubaliano na Real Madrid kuweza kutimiza ndoto za gabriel.” alisema wakala wa Slonina, Garcia.
SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!