Real Madrid Kulipa Kisasi Bila Mashabiki

Real Madrid tayari walipoteza dhidi ya Man City wa kichapo cha 2-1 kwenye mechi iliyopita kabla ya “lockdown” , na sasa wanaamini huu ni wakati muafaka kuelekea kulipa kisasi.

Mechi ya Ligi ya Mabingwa kati ya mabingwa hawa wa LaLiga, dhidi Manchester City walioshindwa kutetea ubingwa wao EPL, itachezwa bila mashabiki.

Kwa mujibu wa Casemiro kucheza katika dimba ambalo halina mashabiki itakuwa ni nafuu katika mpango wao wa kulipa kisasi na kuondoa kuondoa hasara ya kupoteza mechi iliyopita.

Ni mechi ngumu zaidi kwa Real Madrid, wanaosafiri kwenda dimbani Etihad kwenye mechi ya mzunguko pili wa mtoano wa timu 16 kuelekea robo fainali. Real wanataka kubadili matokeo ya 2-1 waliyoyapata kabla ya Corona.

Bila shaka, vijana wa Guardiola wanaenda kuingia dimbani wakiwa na hasira na majuto ya kushindwa kutetea ubingwa wa EPL, na wanaichukulia hii kama nafasi muhimu ya kuendelea kuwika Ulaya. Ni wazi Real Madrid wana kibarua kizito tarehe 8, Agosti.

Wakati Real Madrid wakiwa na mlima wa kupanda Casemiro anaamini kuwa vijana wa Zidane watafaidika na kutokuwepo mashabiki uwanjani.

“Bila mashabiki mchezo ni mwingine kabisa. Utakuwa mchezo mzuri sana na mgumu kwa pande zote, lakini sisi ni Real Madrid na tunafahamu tunayo nafasi ya kusonga mbele.”

“Hawatakuwa na mashabiki hiyo itakuwa nafuu kwetu kiasi. Wachezaji ni wale wale, mwalimu ni yule yule na wote tunaelewa kiwango cha ugumu kitakuwa vile vile kwa kuwa ni timu kubwa.”


Tiketi yako ya kwanza kamwe haiwezi kupoteza ukiwa na Meridianbet. Unarudishiwa 100% ya Tiketi yako ya kwanza.

Ingia mchezoni

40 Komentara

    Tuone Kama watalipa icho kiasi

    Jibu

    Tuone Kama watalipa icho kisasi

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Kweli kabisa itakuwa mchezo mgumu sana huo mana ukizingatia wote wako vizuri hasaivi na wanaendekea vizuri ukiangalia upande wa zidane yuko vizuri hasaivi tumeona dakika za mwisho kabisa anavyo onyesha uwezo wake kupanda mpaka akampita mpizani wake kutoka Barcelona kwa kumzidi point nyingi hivyo anaweza kubadilisha matokeo ya kufugwa 2-1

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Gud .news

    Jibu

    madrid kwa city wajipange sana maana city ni moto wa kuotea mbali wakiamua

    Jibu

    Sidhani kama madrid wataweza kulipa hiko kisasi maana man city wapo miamba tupu

    Jibu

    Nawakubali sana Madrid#Meridianbettz

    Jibu

    Madrid wanaweza

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    itakua mechi ngumu sana

    Jibu

    Mechi ngumu sana acha tuone kama watalipa kisasi au watachapwa tena

    Jibu

    Madrid wanaweza

    Jibu

    Mpira bila mashabiki sijui itakuwaje

    Jibu

    Habali njema kabisa

    Jibu

    Real Madrid inaamini kombe ni lake, kana kwamba haina mpinzani. Mchezo utakuwa mgumu sana#meridianbettz

    Jibu

    Real Madrid nawakubali sana

    Jibu

    Itakuwa poa

    Jibu

    Hakika itakuwa gemu nzur sana

    Jibu

    Tunasubiria kuona km wataweza kulipa kisasi

    Jibu

    Bila mashabiki itakua haileti molari ya mpira maana inasadikika mshabiki ni mchezaji wa kumi na mbili uwanjani.

    Jibu

    Iko poa

    Jibu

    Madrid ni ndoto kuitoa city city ndio kombe wanalolitegemea

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Ngoja tuone kama kweli uefa inauzoefu

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Don’t miss

    Jibu

    Yetu macho kutazama dk 90 Kama kweli atalipa kisasi au atachapwa tena

    Jibu

    Sio mbaya kikubwa kinachotakiwa ni kufanya vizuri

    Jibu

    Mechi itakua babkubwa

    Jibu

    Duuh itakuwa balaaa

    Jibu

    Habar nzur hii

    Jibu

    Hii ni mechi ya kukata na shoka na yenye mvuto mkubwa sana kwenye UEFA

    Jibu

    Duu ilikuwaje bila mashabiki

    Jibu

    Ngoja tusubili tuone itakuaje.

    Jibu

    Raha ya mpira mashabik

    Jibu

    Lazima walipze kisasi

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.