Roma, Milan, Newcastle United na Manchester United wanaripotiwa kuonyesha nia ya kutaka kumnunua mshambuliaji wa VfB Stuttgart Serhou Guirassy.

Kulingana na Footmercato, kumekuwa na mbinu za jumla za kuuliza habari za mchezaji huyo lakini hakuna ofa rasmi kufikia sasa.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
Kuna kipengele cha kutolewa katika mkataba wake wa sasa ambacho kina thamani ya €17.5m na kinaweza kuanzishwa katika dirisha la uhamisho la Januari.

Mshambuliaji huyo wa kati mwenye umri wa miaka 27 pia anaweza kucheza winga ya kushoto na ana mabao matatu katika mechi 12 za wakubwa akiwa na Guinea.
Guirassy alizaliwa na kukulia nchini Ufaransa, amewahi kuzichezea Auxerre, LOSC, FC Koln, Amiens na Stade Rennais kabla ya kuhamia Stuttgart kwa €9m.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.

Amekuwa kificho msimu huu kwa kufunga mabao 16 katika mechi 11 pekee kati ya Bundesliga na Kombe la DFB, pamoja na asisti mbili. Hiyo ni wastani wa bao kila dakika 49 za soka.
Milan wana uhaba wa washambuliaji kiasi kwamba ilibidi kumpa Francesco Camarda mwenye miaka, 15 mechi yake ya kwanza ya Serie A dhidi ya Fiorentina, huku Olivier Giroud akifungiwa kucheza na Luka Jovic amekuwa akikatishwa tamaa tangu kuondoka kwake Viola.


