Romelu Lulaku Ana Furaha Inter

Romelu Lukaku ana furaha zaidi baada ya kurejea Inter na hana mpango wa kurejea Chelsea ambapo yupo kwa mkopo kwa mkataba wa mwaka mmoja utakapokamilika msimu huu. Taarifa zilieleza.

 

Romelu Lulaku Ana Furaha Inter

Romelu, mwenye umri wa miaka 29, hakuwa na msimu mzuri mwaka jana akiwa The Bleus kufuatia uhamisho wake wa Euro milioni 113 kwenda London Magharibi. Lukaku alifunga mabao nane pekee katika mechi 26 za Primia Ligi akishindwa kuonyesha ubora wake huku kukiwa na ukosoaji mwingi.

Baada ya kampeni ngumu, alirejea Inter msimu wa joto kwa mkataba wa mkopo wa mwaka mmoja Euro milioni 8 ambao hauna chaguo la kununua. Kama ilivoelezwa na La Gazzetta Dela Sport, Lukaku amegundua tena furaha yake tena katika jiji la Milan na ana furaha kurejea Inter tena.

The Nerrazzuri ataongeza mkataba wake wa mkopo na Chelsea msimu ujao wa joto, ambao unapaswa kuthibitishwa bila kujali matokeo msimu huu. Uhusiano mkubwa kati ya Rais wa Blues Toddy Boehyl na Rock Nation, Kampuni inayojali maslahi ya Lukaku, umekuwa ukiendelea kwa miaka.

 

Romelu Lulaku Ana Furaha Inter

Kampuni hiyo ilianzishwa na Jay Z na ameleta wachezaji wengi kwa LA Dorgers kwa miaka mingi na kuunda karibu Dola Bilioni 20 za ushirikiano wa biashara.

Msimu wa Romelu ambae ni raia wa Ubelgiji haujakuwa wa mafanikio, huku mchezaji huyo akikosa kucheza kwa takribani mwezi mmoja kutokana na matatizo ya misuli, lakini analenga kurejea kwa wakati kwaajili ya mechi ijayo dhidi ya AS Roma ya Jose Mournho mnamo Oktoba 1, na hali yake imezidi kuimarika.

Acha ujumbe