Baada ya majadiliano ya muda mrefu juu ya ni lini ligi ya EPL irejee, ligi ambayo mwanzo ilipangwa kurejea Juni 12, sasa ni rasmi kuwa ligi hiyo itarejea mnamo Juni 17 baada ya vilabu vyote kukubaliana hivyo.
Ligi hiyo itaanza kwa Aston Villa ya Samatta kuwakaribisha wageni Sheffield United, huku Manchester City wakiwaalika Arsenal pale Etihad Stadium. Mechi hizi mbili ni muendelezo wa kukamilisha viporo ili timu zote katika ligi kuu ziwe zimekwishacheza michezo 29 kisha ligi hiyo itaendelea tena June 19 na 21 katika raundi yake ya 30.
Timu ya Aston Villa anayochezea nyota wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta itarudi uwanjani kuendeleza harakati zake za kujinusuru kutoka katika wimbi la kushuka daraja wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kuraluliwa vibaya na Leicester City katika kipigo cha aibu cha 4 kwa sifuri katika mchezo wao wa mwisho, na ikumbukwe kuwa huo ndiyo ulikua mchezo wa mwisho wa ligi ya Primia kabla haijasimamishwa kwa ajili ya janga la Corona.
Aston Villa walio katika nafasi ya 19 ya msimamo wa ligi yenye jumla timu 20 watakua na kibarua kizito mbele ya Sheffield United ambao wao wapo katika nafasi ya 7 huku wakiwa wamejikusanyia jumla ya alama 43. Hakuna namna nyingine kwa Samatta na wenzie kujinusuru wasishuke daraja ila tu kwa kushinda mchezo huo na mingine itakayowakabili.
Aston Villa wenye jumla ya alama 25 katika michezo 19 waliyocheza mpaka sasa, wamebakiwa na michezo 10 mkononi ambayo wanatakiwa kufanya wawezavyo wabaki katika ligi kuu. Kitu pekee kinachoonekana kuwa kinaweza kuwarahisishia Aston Villa kubaki katika ligi hiyo ni kujikusanyia alama zaidi ya 15 ili wawe na jumla ya alama 40 kujihakikishia nafasi yao katika EPL.
Ni Kwanini Alama 40 Zinaweza Kuwa Salama Kwao?
Katika misimu 23 ya ligi kuu ya Uingereza maarufu kama ‘EPL’ kuna jumla ya timu 20 zilizowahi kushushwa daraja, katika hizo ni timu tatu tu ambazo zilishuka zikiwa na alama kuanzia 40.
Kwa zaidi ya miaka 15 sasa hakuna timu iliyoshuka daraja kutoka Primia ikiwa na alama kuanzia 40. Kumbukumbu zinasema kuwa timu ya mwisho kufanya hivyo ni West Ham United ambao walishuka daraja msimu wa 2002/03 wakiwa na alama 42.
Kwa mazingira hayo, ni wazi kuwa alama 40 ndiyo salama kwa Samatta na wenzie ili waweze kusalia ndani ya ligi kuu, Vinginevyo safari yao ni ya mashaka.


winfrida
sisi mashabiki wa EPL nasubiri kwa hamu yi tarehe 16
Sadick
Litakuwa jambo la kusikitisha endapo Aston Villa itashuka daraja. Hamu yangu ni kuona Liverpool anachukua Ubingwa#meridianbettz
Rehema
Eeeh! Ni hatari sisi mashabiki tunasubili hiyo siku
Hope mwaikuka
Macho modo kwa ajil ya hyo siku
Agness
Tunaisubiri hiyo siku
Devotha
Nasubiri kumuona samagoal77
Neema hassan
Wapenzi wa soka tunasubir kwa hamu
Antony Luseno
Wapenzi wake wanatamani kumwona EPL lakini kuna hati hati ya timu yake kushuka daraja
aisha
Ahsanteni kwa makala safi
Samiah
EPL kuna hati ya Kushuka daraja
Rehema Dickson
wanatamani kumwona EPL lakini kuna hati hati ya timu yake
Tahiya
Anakibarua kizito sana samatta mana timu iko mkiani kabisa na watanzania tuna kiu ya kuendelea kumuona Epl
Adelta
Sisi Kama mashabiki
Tunaisubiri kwa hamu
David pere
Wapige tizi tu maana ninapomuona mtoto wa mbagala huwa nafrahi Sana anpopiga free after zake hatari tupu
Ester mmakasa
Mungu ibariki Aston villa ili samatta na wenziye waendelee kusalia katika ligi.
Elika
Tunaimbea Aston villa ijitahidi isishuke daraja..maana jembe letu mbwana samata tunamtegemea sana.
Mwanaidi
Astonvilla itakuwaje sasa kama itatoka kwenye ligi duh
Theckla
Ni habari mbaya kwa kweli
felister
hamu yangu kubwa kumuona samagoal77
Warda
Wajitahidi tu wasishuke daraja#Meridianbettz
Juliana
Da! Kweli ni habari njema
Salma
Hii sio nzuri kwa upande Wa samatha
Frank Patrick
Kwa Jack Grealish yule dah tutarajie wakishuka tu daraja
Asha
Natak kumuona sama goal atafanya nn epl
Lombo
mambo n moto tumemis sana
mitupio sammagoal
Emmy cleopa
Habari njema
Gabriel
EPL ndo mwake tunaisubir kwa ham
Khadija
Mambo ni Moto#meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Wajitaidi wasishuke daraja
Mariam mtandama
Habari mjema
Amani
Hakuna namna nyingine kwa Samatta na wenzie kujinusuru wasishuke daraja
Caroline
Kitaani panaanza kuchangamkaaa
Mwajuma
Ni vizuri sana kama samatta atakuwa fiti ili aendelea kuwapiga magoli makipa wa timu kubwa
mwakalosi
hahaha jamani arsenal mmsimpigie hesabu na city anafungwa nyingi tu arteta hawezi kumzuia boss wake sama goal king of header ana kamba yake ya header
Hamidu
Samagoal! Pambania timu yko
Bado tunakuhitaji EPL
Shafii
Iko poa hiyo
Povel
Natak kuwaona Aston villa watabaki epl au watashuka daraja thnks meridian bet
Ernest
Tarehe 17 June ndani ya EPL kutanoga sana, Huku Samatta kule Aguero
Magdalena
Samatta piga mpira tunakusubiri kwa hamu zote
Genia Sikaluzwe
Aston villa inaitaji ipambane ili isishuke daraja.
Ester jackson
Daaaah inauma sana wakija shuka daraja mana mbagala ndio wapezi wakubwa wa timu ya mbwana samatta
Neema juma
Hiyo tarehe yenyewe tunaona km inachelewa kufika mambo yanogeee
Kenani
Was was wangu tu ipo kweny Tim kushuka daraja