Sergi Barjuan ametangazwa kuwa kocha muda wa timu ya Barcelona baada ya kocha mkuu Koeman kufunagashiwa vilago mpaka pale atakapotikana kocha anaweza kuchukua mikoba rasmi iliyoachwa na Koeaman.
Taarifa iliyotoka leo alhamisi mchana inasema, “Barcelona imemtangaza aliyekuwa kocha wa Barcelona B, bwana Sergi Barjuan, kuwa kocha mkuu kwa sasa na atachukua majukumu yote ya uongozi na kiufundi kwenye timu ya wakubwa.”

“Nafasi yake ya muda itakoma pale tu klabu itakapo weza kumpata mrithi sahihi wa kuchukua majukumu ya yaliochwa na Ronald Koeman.”
“Raisi Joan Laporta atamtambulisha rasmi Sergi Barjuan kwenye timu ya wakubwa jioni ya hii kabla ya mazoezi kuanza kwenye uwanja wa Ciutat Esportiva
Sergi Barjuan atahudhuria mkutano na waandishi wa habari kesho ijumaa kuanzia majira ya saa saba mchana kwenye ukumbi wa mikutano wa Ciutat Esportiva na kuzungumzia kuhusu mchezo dhidi ya Alaves akiandamana na rais Joan Laporta.
Mchongo wa mkwanja mrefu kutoka kasino bora za mtandaoni za Meridianbet. Mchezo wa Circus Fever unakuweka katika nafasi nzuri ya kuwa mshindi. Furahia kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa meridianbettz.

CHEZA HAPA

