Ya kwanza BISMILLAH, ni kwa Jina la Mwenyezi Mungu mwenye kubariki vitu vyote na kumpa yule amtakae, ni yeye atasema liwalo liwe au lisiwe, ni yeye ataamuwa hata ukipora jua itapotea ili mradi yatimie maandiko
Mwenyezi Mungu aliumba Wanadamu kisha akamuumba Mwanasayansi Albert Einstein, binadamu huyu alisema “everybody is a genius. But if you judge a fish by its ability to climb a tree, it will live its whole life believing that it is stupid”
Basi waambieni Watu waweke kalamu zao vyema, waandae karatasi vyema wanapotaka kumjadili Shomari Salum Kapombe, kuna namna dunia imechoka inalazimisha atokee mtu awe zaidi ya Kapombe lakini bado sana kwasasa na sioni ikitokea karibuni
Naendelea kufurahia kazi ya macho yangu kama Shomari anaweza kucheza beki ya kulia na akateleza kama Anaconda na misitu ya Amazon, naendelea kutabasamu nikimuona kwenye eneo la Kiungo akipokea pass kama Mafikizolo na kuzipiga kama kinanda cha Mozart
Enyi Mashabiki kuna dhambi zinaepukika ukiachana na dhambi kuu ya kudhini, basi hii dhambi ya kuamini kuna mbavu ya kulia kama Shomari tujiepushe nayo, tuendelee kufurahia kwakuwa watu kama hawa huzaliwa mara chache, kwenye nchi chache na kwa nyakati chache
Wapo vijana wanakuja ila bado Shomari ni Marking scheme yao, unataka kuwa bora mtazame Shomari, unataka kucheza kwa muda mrefu basi mtazame Shomari, umewahi kupitia majaribu ya soka na hujui utashinda vipi? Basi mpigie simu Shomari, atakwambia kila kitu
Acha niendelee kufurahia kazi ya macho yangu, kama ambavyo Madaktari wa Afrika Kusini walivyopitisha kisu kwenye mwili wa Shomari kumaanisha kuwa mpira bado unamdai, kama ambavyo alijiondoa Stars na kurudi tena kumaanisha kuwa nchi bado inamdai vingi.
Kila Binadamu ana ubora wake ila tukimlaumu Samaki kwanini hapandi mtini, basi Samaki ataishi maisha yake yote kujua kuwa hana akili, kifupi alimaanisha kila Mtu ana ubora na upungufu wake na sio lazma afanane na mwingine, alimaanisha hivyo Albert Einstein
Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!
David Pere
Wapo vijana wanakuja ila bado Shomari ni Marking scheme yao, unataka kuwa bora mtazame Shomari, unataka kucheza kwa muda mrefu basi mtazame Shomari, umewahi kupitia majaribu ya soka na hujui utashinda vipi? Basi mpigie simu Shomari, atakwambia kila kitu
Issa
Kapombe ni mtu hatari
Adelta
Shomari Yuko makini na kazi yake
Neema juma
Shomari kijana yuko vzr
Magdalena
Kapombe yupo vizuri
Ernest Kimeru
Salute kwa Mwandishi
Dorophina
Nice update
Hopemwaikuka
Imeeleweka
Lydia Emmanuel Magoti
Abari nzuri
Sania
Kapombe yuko poa
Sarah
Kapombe Yuko vizuri
Zahara Omary
HAbar nzur snaa
warda
Shomar kama shomar