Klabu ya Simba leo inaingia vitani kuhakikisha inapata alama zote tatu leo dhidi ya klabu ya CS Sfaxien kutoka nchini Tunisia kwenye mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa.
Simba wanazihitaji alama tatu za leo kwa udi na uvumba kwakua wanajua zitawaweka kwenye mazingira mazuri ya kufuzu hatua ya robo fainali ya kombe la shirikisho barani Afrika, Kwnai wakiwafanikiwa kukusanya alama zote leo watafikisha jumla ya alama sita hivo watakua na alama tisa za kuzipambania katika michezo mitatu iliyobaki na kufanya kazi isiwe ngumu zaidi.Wekundu wa Msimbazi kama ilivyokua kawaida yao mara nyingi wanapokua kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa wamekua wakipata matokeo mazuri na leo wanawakaribisha Watunisia kwenye uwanja huo ambao timu nyingi vigogo wamewahi kucheza hapo na kuambulia vichapo, Hii ikiwa ni dalili nzuri kwa klabu hiyo yenye rekodi nzuri kwenye michuano ya Afrika.
Klabu ya CS Sfaxien mpaka sasa inashika mkia kwenye kundi ambapo wamecheza michezo miwili na kupoteza michezo yote na leo wanacheza ma klabu ya Simba ambao wamepoteza mchezo mmoja na kushinda mmoja, Hivo ni mchezo muhimu kwa timu zote Sfaxien wanaioana kama nafasi ya kufufua matumaini huku wekundu wa msimbazi wenyewe wakiona nao ni mchezo ambao unaweza kuwafanya kukaa kwenye nafasi nzuri ya kufuzu.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.