Habari mbaya kwa klabu ya Spezia inayocheza Serie A. FIFA imeifungia klabu hii kufanya usajili wowote kwa madirisha mmanne ya usajili.
Spezia wanakumbana na adhabu hii kufuatia uvunjifu wa sheria za FIFA na mamlaka za uhamiaji nchini Italia. Hili lilifanyika katika usajili wa wachezaji wadogo kutoka Nigeria. Sambamba na kufungiwa usajili, klabu hii pia imepigwa faini ya £393,000.

Hii ni habari mbaya zaidi kwa mchezaji wa zamani wa PSG na Barcelona, Thiago Motta ambaye alipewa kibarua cha kuwa kocha wa klabu hiyo wiki iliyopita.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!


