Tetesi za Soka Barani Ulaya.

 

Tetesi zinasema, Manchester City iko kwenye nafasi nzuri ya kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Erling Braut Haaland, mshambuliaji huyo wa mwenye umri wa miaka 21, atapatikana kwa ada ya £68m katika majira ya joto.

Tetesi zinasema, Mlinzi wa Chelsea Cesar Azpilicueta, 32, ana mkataba wa kujiunga na Barcelona bure wakati mkata wa mlinzi huyo wa Hispania utakapomalizika wakati wa majira ya joto.

Edinson Cavani anatarajiwa kuondoka Manchester United wakati mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu na mshambuliaji huyo wa Uruguay, 34, angependelea kutimkia Hispania kuliko kurejea nyumbani Amerika Kusini.

 

Mtendaji mkuu mpya wa Manchester United, Richard Arnold anaunga mkono juhudi za Ralf Rangnick za kumnasa kocha wa Ajax Erik ten Hag kuwa meneja mpya wa timu hiyo, licha ya wachezaji wengi kumtaka kocha wa Paris St-Germain Mauricio Pochettino.

Tetesi zinasema, Liverpool inatarajia kumpa mkataba mpya mshambuliaji wa kibrazil Roberto Firmino, 30.

Kocha wa Leicester Brendan Rodgers amezidi kuchochea uvumi kwamba kazi yake ijayo itakuwa kwenye mji wa Manchester, baada ya kutafuta makazi mapya karibu na eneo la soka la Cheshire.

Lyon wanaendelea kusubiria majibu ya Jason Denayer, 26, kama atakubali ofa yao a mkataba mpya, huku Barcelona, Newcastle, Juventus na Napoli wakimfuatilia mlinzi huyo wa Ubelgiji, ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu.

 

Barcelona wanajiandaa kulipa £50.2m kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa Nabil Fekir, ingawa klabu ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 28, Real Betis inataka £66.2m.

Tetesi zinasema, Borussia Dortmund wanaamini watafikia makubaliano ya kumsajili mshambuliaji wa ujerumani Karim Adeyemi, 20, kwa mkataba wa miaka 5 kutoka Red Bull Salzburg.

Paris St-Germain hawana shaka na wako tayari kiungo mholanzi Xavi Simons, 18, kusaini mkataba mpya kabla mkataba wake wa sasa kumalizika mwishoni mwa msimu huu.


KASINO YA MTANDAONI: EMOTICOINS SABABU YA KUVUNA ZAIDI.

Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.

senegal, Senegal Mabingwa AFCON 2021., Meridianbet

CHEZA HAPA.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.