Tetesi zinasema, Paul Pogba alikubaliana masharti binafsi na Manchester City lakini alibadili maamuzi baada ya kuhofia kulaumiwa na kudhihakiwa na mashabiki wa Manchester united.
Nyota wa Paris St-Germain Kylian Mbappe atatangaza uamuzi wake siku ya Jumapili huku mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 rais wa Ufaransa akihusishwa kwa muda mrefu na taarifa za kuhamia Real Madrid.

Tetesi zinasema, Arsenal, Newcastle na Everton wanataka kumsajili mshambuliaji Barcelona Mholanzi Memphis Depay, 28.
Tetesi zinasema, Tottenham wanataka kumsajili kwa mkopo mlinzi wa Ufaransa Clement Lenglet, 26, ambaye yuko tayari kuondoka Barcelona.
Mshambuliaji wa Bayern Munich, Robert Lewandowski, 33 anataka kujiunga na Barcelona pekee msimu huu wa joto, huku akipewa mkataba wa miaka 3 kutua Camp Nou.

Tetesi zinasema, Manchester United wamepewa ofa ya kumsajili beki wa Barcelona, Mmerekani Sergino Dest, 21 akitajwa kuchukua nafasi ya Aaron Wan-Bissaka, 24, ambaye ataruhusiwa kuondoka msimu huu.
Divock Origi anatarajiwa kujiunga na AC Milan wakati mkataba wake na Liverpool utakapoisha msimu huu, huku mshambuliaji huyo Mbelgiji mwenye umri wa miaka 27 akiwa kashakubaliana na Milan.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


