Tetesi zinasema, Barcelona wamemwambia mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri Mohamed Salah, 29, kwamba anaweza kujiunga nao kwa uhamisho wa bure wakati mkataba wake na Reds utakapomalizika msimu ujao.
Tetesi zinasema, Liverpool wamejiondoa kwenye kinyang’amyiro cha kumnunua kiungo wa kati wa Barcelona mwenye umri wa miaka 17 raia wa Uhispania, Gavi.
Kiungo wa kati wa Serbia Nemanja Matic, 33, atajiunga na Roma kwa uhamisho huru mkataba wake utakapomalizika Manchester United mwisho wa mwezi huu.
Tetesi zinasema, Benfica wana matumaiani ya kufikia makubalianao na mchezaji wa kimataifa wa zamani wa Ujerumani Mario Gotze, 30, kuhusu uhamisho kutoka PSV.
Chelsea huenda ikasaidia kumshawishi mchezaji wao Declan Rice, 23, kurejea nyumbani kutoka klabu ya West Ham kwa kumpatia kiungo huyo wa kati wa Uingereza fulana nambari 41 mgongoni.
Mkurugenzi wa michezo wa Barcelona Mateu Alemany anatazamiwa kuelekea Uingereza wiki hii kuanza mazungumzo na Leeds kuhusu mpango wa kumnunua mshambuliaji wa Brazil Raphinha, 25.
Beki wa Uholanzi Matthijs de Ligt, 22, amethibitisha kuwa yuko kwenye mazungumzo na Juventus kuhusu mkataba mpya lakini bado hajafanya maamuzi.
SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!