Timo Aitaka Liverpool Apiga Chini Ofa ya Bayern

Timo Werner ametangaza kuwa anapendelea kuhamia kwenye ligi nyingine baada ya kuthibitisha kuwa hana nia ya kujiunga na Bayern Munich.

Ripoti nchini Ujerumani wiki hii zilidai nyota huyo wa RB Leipzig alikuwa ameamua kupiga chini ofa Bayern, akisisitiza ni bora kuhama Bundesliga na kutua klabu nyingine kuliko kubakia Ligi hiyo hiyo na kujiunga na klabu tofauti.

Werner, ambaye ameripotiwa kupokea ofa kutoka Chelsea na Manchester United, ana kifungu cha uhamisho kwenye Mkataba wake cha pauni milioni 50 na anapendelea kujiunga na Liverpool kwenye dirisha linalofuata la uhamisho. Werner alisema: “Changamoto kwenye ligi ya nje ingenivutia badala ya kuhamia Bayern.”

Chelsea na United pia wanamsaka mshambuliaji huyo, lakini wanajua kuwa Liverpool ndio wanaongoza mbio hizo za kuwania saini yake. Werner amejidhihirisha kama mmoja wa Washambuliaji hatari zaidi barani Ulaya, akiwa na magoli 27 katika mashindano yote kwa klabu yake ya Leipzig msimu huu.

26 Komentara

    Hyo ni jesh awez kutoka hapo

    Jibu

    Bora uende man u mzee baba.

    Jibu

    Amengalia mbal ukiangalia England ndo lig inayopendwa dunian

    Jibu

    Ameangalia mbali zaidi hili akarisakate soka England

    Jibu

    Yupo vzr..anatakiwa aje man utd

    Jibu

    England panakufaa

    Jibu

    England mbona pazuri tu we hamia

    Jibu

    Bora uende tu uko England

    Jibu

    Kaangalia pesa na ligi bora

    Jibu

    Aangalie masilahi na asiache kujituma

    Jibu

    Jamaa anajua Sana kufumania nyavu ni bora aje EPL pale aje kuleta chachu ya magoli England

    Jibu

    Ana gut za kukataa offer ya munich kweli

    Jibu

    👍

    Jibu

    Kubadili mazingira ni Jambo la msingi sana hata Mimi nitafurahi kama Werner atahamia ligi nyingine

    Jibu

    Tunamukaribisha Stamford Bridge

    Jibu

    nenda England ligi yenye ushindani dunian

    Jibu

    Aje tu

    Jibu

    Mashabiki wa man utd tunamsubiri kwa hamu..

    Jibu

    Maslah muhim

    Jibu

    Huyu anataka kufanya kazina klop alishawai kusema

    Jibu

    Angalia maslahi mzee babaeeel

    Jibu

    Mfanyakazi hanaonekana tu

    Jibu

    👌

    Jibu

    Tunamkaribisha sana

    Jibu

    Tunasubiri

    Jibu

    Bola aende man#meridianbettz

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.