Kocha wa klabu ya Manchester City, Pep Guardiola alisema kwamba hatojali lolote lile endapo kikosi chake kingemaliza msimu bila kuwa na taji lolote. Kocha huyo ametasema hayo kwa kuona kwamba hana wasiwasi wa namna ambavyo wengi wanahisi hatakuwa na amani kunyanyua kikombe ndani ya msimu huu kutokana na kuwa na matokeo mabovu ambayo hayaendani kabisa na kasi yake ya msimu uliopita.
Kocha huyo aliona kwamba hadi sasa mataji ambayo aneyanyanyua mfukulizo na klabu hiyo ni kipomo tosha kabisa cha kuweza kuaminisha kwamba anaweza kazi yake hiyo. Amenyanyua kombe la ligi mara mbili mfululizo akiwa na kikosi hicho na makombe mengine ya ndani. Kwa hiyo suala hilo halimpi wasiwasi.
Ramani hiyo imeanza kuonekana mara baada ya kocha huyo kuona kwamba watu wameanza kumwangalia kwa namna nyingine kutokana na kupoteza mechi yake mbele ya klabu iliyopanda ligi msimu huu pia mara baada ya kuwa na mwenendo ambao kikosi chake kinaonesha kusuasua sana ndani ya ligi hiyo.
Maajabu ambayo hayatasahaulika kwa kocha huyo ni kunyanyua kombe akiwa na alama nyingi sana katika ligi ambazo zilikuwa 98 jambo ambalo kwa miaka ya karibu lilikuwa kama historia na mapinduzi makubwa katika soka la Uingereza. Hivyo, kwake hilo sio changamoto na aliliona halina nguvu kumpa mawazo sana.
Jimgine ambalo kocha huyo alijaribu kulizungumzia ni juu ya hali halisi ilivyo kikosini hapo kwa sasa kwamba sio rahisi sana kutokana na kuanza msimu kwa kuwa na wachezaji ambao ni majeruhi, tena wachezaji ambao ni muhimu sana katika kikosi chake cha kwanza; hivyo hilo ni jambo ambalo kwake bado ni changamoto kiasi fulani.
Akiwa kama kocha pia amezungumzia suala la kuwa na wach3zaji wa aina moja katika misimu kadhaa mfululizo kwamba nalo huwa linashusha ushindani kwa sababu kikosi hicho huwa tayari kimeshinda kila kitu na kuona kwamba ni hali ya kwaida sana hata pale wanapotokea kukosa ubingwa fulani.
Lakini mbali na hilo ametahadharisha kwamba hilo sio sababu ya yeye kukata gamaa ya kufukuzia ubingwa bali ni onyo tu la kawaida ambalo ameliweka kwa wale wanaoona kwamba kocha huyo huenda ameanza kukubali hali halisi ya ligi kwa msimu huu. Kwamba atashindwa kufanya vyema kabisa.


Sadick
Ligi ya ushindani ni ile kila msimu kunakuwa na Bingwa tofauti. Sio afya kwa ligi kuwa na Bingwa yuleyule kama iliyo Serie A Juventus wamechukua Ubingwa misimu 9 mfululizo#meridianbettz