Kuongezeka kwa wimbi jipya la maambukizi ya covid19, kumepelekea mchezo wa Uefa kati ya Bayern Munich na FC Barcelona kuchezwa bila ya mashabiki.
Imeripotiwa kuwa, jiji la Munich ni miongoni mwa maeneo yaliyoathirika sana na maambukizi ya Covid19 na hivyo, jitihada za makusudi na haraka zimechukuliwa ili kulinda usalama wa wananchi wake.

Huu ni mchezo wa 6 kwenye hatua ya makundi kunako mashindano ya Uefa. Bayern ameshafuzu hatua ya mtoano na sasa, kazi ipo kwa Barca na Benfica ambao wote wanaitafuta nafasi ya kufuzu mtoano.
Mchezo wa kwanza ulichezwa pale Camp Nou ambapo Bayern alishinda 3-0. Ili Barca afuzu hatua ya mtoano, anahitaji kuwafunga Bayern. Matokeo ya sare au Barca kupoteza, yatawapa nafasi Benfica nafasi ya kutinga hatua ya mtoano endapo watawafunga Dynamo Kyiv.
Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.


