NBA 2021/22 inaendelea kupamba moto viwanjani. Rekodi zinawekwa na kuvunjwa kila uchwao. Sasa ni zamu ya Phoenix Suns.
Suns walikua uwanjani kuchuana na Golden State Warriors katika mchezo wa 19 kunako NBA msimu huu. Stephen Curry ameongoza timu iliyopeleka maumivu Suns kwa kupachika pointi 23 kati ya 118 zilizowapa ushindi Warriors (Suns walipata pointi 96).
Safari ya Suns ya ushindi kwenye michezo 18, imekatishwa na Warriors. Kule Los Angeles pia kulikua na mtanange wa majirani – LA Clippers vs LA Lakers.

3 pointers 2 za dakika za mwisho kutoka kwa Luke Kennard, zimewatosha Clippers kuwapasua Lakers kwa pointi 119-115. NBA ilinoga zaidi kwa mchezo wa Philadelphia 76ers vs Atalanta Hawks, Joel Embiid akiwatoa 76ers kimasomaso kwenye sekunde za lala salama. Pointi 98-96 zinamaliza mchezo.
Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.


