Angel Di Maria amesema kwamba yeye ni rafiki mkubwa Lionel Messi nje ya uwanja lakini pia wametengeneza muungano mzuri ndani ya uwanja katika timu ya taifa ya Argentina na PSG.

Di Maria ambaye aliwahi kuichezea Real madrid alikiri kwamba alikuwa amekaribia kujiunga na Barcelona mapema wakati wa kazi yake na winga huyo amekuwa akihusishwa kujiunga na Barca baada ya dili yake ya sasa kuisha huko Parc des Princes.
“Nilikuwa karibu sana kwenda Barcelona,” Di Maria aliambia TNT Sports.
“Kama ningeenda ingekuwa ni kucheza naye tu, alipoondoka nilifurahi, ni jambo bora zaidi lililonipata, kucheza naye ni ndoto niliyoota, ni kitu cha kipekee.
“Mtoto ni wa ajabu, ni hatari. Saba Ballon d’Ors ni ajabu. Ni nusu ya kazi yake na tuzo nyingine zote za Ballon d’Or waliyopewa wengine, ikiwa ni tuzo ya bora zaidi duniani, basi. wangempa yeye Messi”
Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.


