Uefa Kuanza Kutimua Vumbi Wiki Hii.

Ule muda wa mashabiki wa soka kuanza kuburudika na mashindano ya Ligi ya Mabingwa (Uefa), umewadia! Timu bora barani Ulaya kuanza kupepetana wiki hii.

Baadhi ya timu zitakua na sura mpya kwenye vikosi vyao wakati vingine vikiwa kama vilivyokuwa msimu uliopita. Messi ndani ya PSG, Ronaldo ndani ya Man United, Grealish ndani ya Man City, Lukaku ndani ya Chelsea, Sabitzer ndani ya Bayern Munich, Alaba ndani ya Real Madrid na wengine wengi!!

Macho ya wengi yatakua pale Camp Nou ambapo Barcelona itawaalika Bayern Munich. Huu ni mchezo ambao Barca anaingia uwanjani akiwa na kumbukumbu ya kufungwa 8-2 na Bayern kwenye mashindano Uefa msimu uliopita. Kipigo kitaendelea au Bayern wataambulia patupu?

Memphis Depay (FC Barcelona)

Liverpool atawaalika AC Milan pale Anfield. Hizi ni timu mbili zenye historia ya heshima kwenye mashindano haya. Milan watamkosa Zlatan Ibrahimovic ambaye amepata majeruhi, huku Liverpool wakimkosa chipukizi wao – Elliot ambaye naye ni majeruhi.

David Alaba kuipeperusha bendera ya Real Madrid akitokea Bayern Munich.

Inter Milan uso kwa uso na Real Madrid kwa mara nyingine msimu huu. Timu hizi zilikua kwenye kundi moja msimu uliopita na zimekutana tena msimu huu. Nani kuondoka na pointi 3 muhimu kwenye mchezo huu wa kwanza?

Mabingwa watetezi wa Uefa – Chelsea, watawaalika Zenit pale Stamford Bridge. Safari ya kutetea ubingwa inaanza rasmi!

Romelu Lukaku (Chelsea)

Unaweza kutandaza tiketi yako ya ushindi kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa kwa kubashiri na Meridianbet. Bofya hapa kuingia mchezoni.


MKWANJA NJE NJE NA DISCO FUNK

Unaanzaje siku yako na kuimaliza bila kupitia katika kasino bomba za meridianbettz, mchezo mashuhuri wa Disco Funk unaweza kukufanya uwe mshindi leo hii.!

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.