Manchester United inaripotiwa kuwa tayari kufanya uhamisho wa walinzi wawili wapya wa kati katika usajili wa msimu huu wa joto, wakati kikosi cha Ole Gunnar Solskjaer kinajiandaa kuivaa changamoto ya taji la Ligi Kuu msimu ujao.
Mashetani Wekundu wamekubali mpango wa kumsajili Jadon Sancho kutoka Borussia Dortmund, wakati Raphael Varane wa Real Madrid anaaminika kuwa ndiye anayeongoza kwa klabu huyo nyuma ya pazia.
Kwa mujibu wa Manchester Evening, Man United wanapiga hatua kwa kasi kwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa, ambaye anaaminika kuwa anataka kuondoka mji mkuu wa Uhispania msimu huu wa joto.
Hata hivyo, ripoti hiyo inadai kwamba mabingwa hao wa Uingereza wa mara 20 wanafikiria kumsajili beki mwingine wa kati, huku Pau Torres wa Villarreal pia akiwa na nia ya saini ya Varane.
Eric Bailly anadaiwa kuwa anaweza kutumiwa kwa dili la kubadilishana na Torres, ambaye kwa sasa anashiriki Euro 2020 na Uhispania.
Axel Tuanzebe anatarajiwa kuondoka Old Trafford kwa mkopo msimu ujao, wakati Phil Jones hatma yake ikiwa na sintofahamu hapo United hata kama ataweza kupona jeraha la muda mrefu.
IcyGems kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet. Ndio, ukiwa kwenye nyumba ya mabingwa, ndipo utakapoufurahia ubora wa Kasino ya Mtandaoni sambamba na kushinda kwa ushindi mkubwa! Ishi na hii, IcyGems!