Everton kuwapiga Gepu Arsenal kwa Ben White

Everton wameripotiwa kuwaarifu Brighton & Hove Albion kuwa wako tayari kulipa pauni milioni 50 kumsajili Ben White wakati wa msimu huu wa usajili wa majira ya joto.

Mchezaji huyo wa miaka 23, ambaye sasa yuko na kikosi cha England kwenye Euro 2020, aliwashawishi sana Everton wakati wa kampeni ya 2020-21, akishiriki mara 39 kwenye mashindano yote.

Arsenal inaendelea kuhusishwa sana na White, lakini inaeleweka kwamba Gunners wanajitahidi kupata ada inayotakiwa kufungua mazungumzo na mawasiliano na beki huyo wa kati.

Everton Kuungana na Real Madrid Kuchuana na Arsenal kwa Ben White
Real Madrid na Arsenal pia wanahusishwa na Ben White

Kwa mujibu wa The Sun, Everton, chini ya maagizo ya kocha mkuu mpya Rafael Benitez, wameiambia Brighton kuwa wako tayari kulipa pauni milioni 50 kwa Muingereza huyo.

Ripoti hiyo inadai kuwa White kwa sasa anazingatia majukumu yake huko Euro 2020 lakini anafahamu kuwa kuna vita ya kuinasa saini yake kabla ya msimu wa 2021-22.

Mlinzi huyo amebakiza miaka mitatu kukamilisha mkataba wake na timu ya Graham Potter.


KUSANYA PESA HAPA!

IcyGems kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet. Ndio, ukiwa kwenye nyumba ya mabingwa, ndipo utakapoufurahia ubora wa Kasino ya Mtandaoni sambamba na kushinda kwa ushindi mkubwa! Ishi na hii, IcyGems!Meridianbet

INGIA MCHEZONI

Acha ujumbe