Usajili wa Donny Van De Beek haukutarajiwa miongoni mwa mashabiki wengi wa Man United. Licha ya kucheza mechi chache, Donny ni kama anaendelea kuonesha ubora wake ndani ya United.
Kwenye Ligi ya Mabingwa, Van De Beek amecheza mechi zote za Man United (4 mpaka sasa) katika nafasi mbalimbali. Mchezo dhidi ya Istanbul Basaksehir Donny alicheza kama namba 8 akisaidiana na Fred aliyecheza kama kiungo mkabaji.
Ni kati ya michezo ambayo kiungo huyo raia wa Uholanzi ameendelea kuonesha uwezo wake mkubwa wa kutawala mchezo na kuongoza mashambulizi. Anazitumia vizuri nafasi anazozipata na pia anatengeneza nafasi kwa wachezaji wengine awapo uwanjani.

Je, kuonesha kiwango safi kwenye michezo ya Ligi ya Mabingwa kutampatia Van De Beek namba ya kudumu kwenye kikosi cha Man United?.
Kocha – Ole Gunnar Solskjaer alizungumzia maendeleo ya Donny na Edinson Cavani ndani ya kikosi chake.
Akizungumza na BT Sports, Solskjaer alisema “wote wameanza kuzoea maelekezo ya namna tunavyowataka wacheze – Donny anaweza kucheza kwenye nafasi mbalimbali na Edinson ni namba 9 mwenye staili ya zamani, kitu ambacho hatukuwa nacho kwa muda na nilifurahishwa na namna Martial alivyocheza upande wa kushoto.”
Donny alipata nafasi ya kuzungumza na MUTV ambapo alisema “Ulikuwa ni mchezo mzuri. Kwenye baadhi ya michezo ninacheza namba 10, muda mwingine kocha ananihitaji nicheze katika nafasi za kuutawala mchezo, hiyo ni sawa kwangu, muda mwingine nilipokuwa Ajax nilikuwa ninacheza kwenye nafasi hiyo hivyo hakuna tatizo katika hilo.”
Donny anapambia namba katika kikosi cha Man United akichuana na wachezaji kama Paul Pogba, Bruno Fernandes, Juan Mata, Fred, Scot McTominay na Nemanja Matic katika orodha ya viungo wa timu hiyo.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.



Adelta
Van dee Yuko vizuri na anajitahidi kutufurahisha mashabiki
Mwajumah
Namkubali sana Van dee anajua anachokifanya akiwa uwanjani
Caroline
Van De beek hongera sana.ulionyesha kiwango kikubwa kwenye ligi ya mabingwa.endeleza moto wako huo huo
magdalena
van de beek yupo vizuri sana
Sania
Van de beek yuko poa
Rahma
Van de beek mtu makin
Sauda
Jamaa anajituma.
Ester jackson
Kama akiendelea na mashbulizi mzuri Van De Beek anaweza kupata namba ajitahili kwa hilo
Nasra
Huyu jamaa juhudi zake zinaonekana
Khadija
van dee yupo vzr sana
Fatina mfingi
Jamaa yuko vizur sana
Hopemwaikuka
Pambana mwana mpaka kieleweke
aisha
Anajielewa sana huyu jamaa sio powa
Angelina
Nice update
Povel
Van de beek ni mmoja ya viungo bora waliotokeah ndani ya united mashabik na wapenzi wa united wanategemeah makubwa kutokA kwa van de beek msimu huu
Dorophina
Van de beek anamchango mkubwa sana katika kikosi cha man u
Saupha mohamed
Van de beek yupo vizuri sana
Issa
De beek anatisha sana
Sadick
Uzuri wa Ole kila mchezaji anayemnunua anamchezesha ingawa anakuwa hana uhakika wa namba. Man ilitakiwa kusajiri beki sio nafasi ya kiungo
Gabriel
van de beek yupo vizur
neema hassan
Mchezaj mahiri awapo uwanjan
samiah
Gud
Latifa juma mohamed
Namkubali sana Van dee anajua anachokifanya akiwa uwanjan
Shakila mrope
Good
Tatu
Van de yupo vizuri
Samira
Van bado ni kiungo makini sana pale man u
Lydia Emmanuel Magoti
Van yupo vizuri dogo huyo
warda
Yuko poa sana
Chiku
Ajawai kosea